KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, February 5, 2014

Frank Lampard,Oscar na Ramirez wapinga makahaba kombe la dunia nchini Brazil

Wachezaji mashuhuri katika ligi za soka za Uingereza na zile za Brazil wanajiunga na kampeni ya kuwaonya mashabiki dhidi ya kuwatumia makahaba watoto wakati wa michuano ya kombe la dunia nchini Brazil baadaye mwaka huu.
Wachezaji wa kilabu ya Chelsea Frank Lampard,Oscar na Ramirez wanaunga mkono kampeni hiyo inayoshirikisha kitengo cha kukabiliana na uhalifu nchini Uingereza pamoja na serikali ya Brazil.
Kampeni hiyo inawaonya wafuasi wa Uingereza kwamba watakabiliwa na tisho la kushtakiwa iwapo watalipa ili kulala na wasichana walio chini ya umri 18.
Taifa la Brazil linakadiriwa kuwa na nusu ya milioni ya idadi makahaba watoto wanaosimamiwa na magenge ya uhalifu na kuna hofu kwamba idadi hiyo itaongezeka wakati wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment