KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, February 5, 2014

Fulham wang'olewa FA Cup na Sheffield United

Klabu cha ligi ya Premier, Fulham, walizidi kufedheheshwa pale walipongolewa kutoka kombe la FA na Sheffield United wanaocheza daraja ya tatu Uingereza.
Washikilia mkia hao wa Premier walichakazwa 1-0 nyumbani kwao Craven Cottage kwenye mechi iliyolowa kutokana na mvua kali.
Kivumbi hicho kilielekea kuamuliwa na mikwaju ya penalti baada ya ukosefu wa nafasi wazi za kufunga na kuzembea kwa mashambulizi hadi Shaun Miller alipoibuka nyota dakika ya 120.
Miller alitia kizimbani kupitia kichwa baada ya kunganishiwa na mwenzake Harry Maguire huku United wakiongeza Fulham kwa kaburi lao la timu za Premier baada ya kuondoa Aston Villa katika raundi ya tatu ya kombe hilo.
United wanajiandaa kuchuana na Preston North End au Nottingham Forest katika raundi ya tano huku Fulham, walioanguka hadi nafasi ya mkia katika Premier baada ya kushindwa mechi nne mtawalia wakikondolea masaibu.

No comments:

Post a Comment