KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, March 20, 2014

Ligi ya England: Vita ya maneno kumalizwa Jumamosi baina ya Wenger na Mourinho, yaani 'bingwa wa kufeli dhidi ya mjinga aliyekosa heshima'

Arsene Wenger ana nafasi ya kumnyamazisha Jose Mourinho Jumamosi timu yake ya Arsenal itakapozuru Stamford Bridge ikilenga kupokonya Chelsea udhibiti wa kinyang’anyiro cha kushinda Ligi ya Premia.

Hakuna njia bora zaidi ya kusherehekea mechi ya 1000 akiwa kwenye usukani Arsenal kushinda kuvunja rekodi ya kutoshindwa nyumbani katika ligi ambayo anajivunia mdosi huyo wa Chelsea ambaye mwezi uliopita alipuuzilia mbali na kumtaja kuwa “mtaalamu wa kufeli”.

Vita vya maneno vimekuwa vikiendelea kwenye mbio za ligi ya premia lakini ni uwanjani ambapo alama hushindwa na kupotezwa. Matokeo ya debi hiyo ya Jumamosi huenda yakawa na umuhimu mkubwa kuamua nani atakwua mshindi Mei 11.
Chelsea walionekana kudhibiti vyema mbio hizo hadi wikendi iliyopita waliposhindwa 1-0 na Aston Villa. 

Ushindi wa Liverpool, Arsenal na Manchester City ulifanya mambo kuwa magumu zaidi kileleni.
 
Timu hiyo ya Mourinho bado ina uongozi katika msimamo wa ligi ikiwa na alama nne mbele ya Arsenal na Liverpool, ingawa wote wawili wana mechi moja ambayo hawajacheza, huku City walio alama sita nyuma ya Chelsea wakiwa na mechi tatu za kucheza.

City watakuwa nyumbani kukabiliana na klabu ya Fulham inayoshika mkia katika ligi Jumamosi, huku Liverpool wakisaka ushindi wao wa sita mfululizo ugenini kwa Cardiff City ambao wanapigana kukwepa shoka la kushushwa daraja.

Wenger alitaja matamshi ya Mourinho kuwa ya “kijinga” na ya “kukosa heshima” mwezi jana baada ya kocha huyo Mreno kufanyia mzaha ukame wa mataji wa misimu minane wa Mfaransa huyo.

"Ninaogopa kufeli? Yeye ni mtaalamu katika kufeli. Mimi hapana. Kwa hivyo mtu akidhani kwamba hajakosea, na kwamba naogopa kushindwa, ni kwa sababu huwa sishindwi mara nyingi,” akasema Mourinho.

Wenger alikuwa ameanzisha majibizano hayo alipouliza maswali kuhusu nia ya Mourinho kusema timu yake ni “farasi mdogo” kwenye mbio dhidi ya Manchester City ambao ni "jaguar".

Arsenal walionekana kuteleza baada ya kushindwa mara mbili mfululizo katika ligi, lakini ushindi wa 1-0 dhidi ya wapinzani wao kutoka London kaskazini Tottenham Hotspur wikendi iliyopita ulifufua matumaini yao ya kushinda taji hilo mara ya kwanza tangu 2004 – mwaka ambao Mourinho alifika mara ya kwanza London akijiita “the Special One” yaani Yule Mteule.

Ushindi Stamford Bridge, ambapo Mourinho hajawahi kupoteza mechi ya ligi, utawaweka alama moja kutoka kileleni wakiwa na mechi moja ambayo hawajacheza, jambo ambalo litakuwa kibarua ikizingatiwa kwamba Jack Wilshere, Aaron Ramsey, Theo Walcott na Mesut Ozil wanauguza majeraha.

No comments:

Post a Comment