Timu tatu za Hispania zimefanikiwa kucheza fainali mbili tofauti za mashindano yenye hadhi ya juu barani Ulaya mwaka 2014.
Timu hizo mahasimu zimefikia hatua hiyo baada ya
Real Madrid kuwachabanga waliokuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo
Bayern Munich ya Ujerumani kwa jumla ya mabao 5-0. Real Madrid ilipata
ushindi wa bao 1-0 nyumbani, huku ugenini ikiisambaratisha Bayern magoli
4-0.
Nayo Atletico Madrid baada ya
kushindwa kuifunga Chelsea katika uwanja wa nyumbani kwa kutoka suluhu
ya 0-0, katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali katika uwanja wa
Stanford Bridge jijini London, Chelsea ilikiona cha moto kwa kuchabangwa
magoli 3-1.
Hivyo vita vya ndugu hao Real Madrid na Atletico
Madrid vitapiganiwa ugenini katika uwanja wa Estádio do Sport Lisboa e
Benfica, ujulikanao pia kama Estádio da Luz (uwanja wa mwangaza)mjini
Lisbon, Ureno, Jumamosi tarehe 24 Mei 2014.
Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1967, fainali za kombe la ligi ya mabingwa la UEFA zinafanyika mjini Lisbon.
Katika fainali nyingi za kombe la ligi ya
Europa, Sevilla ya Hispania inapambana na Benfica ya Ureno mchezo
utakaopigwa katika dimba la Turin, nchini Italia Jumatano tarehe 14 Mei
2014.
Sevilla imefuzu kucheza fainali hizo baada ya
kuwatoa ndugu zao Valencia katika mchezo wa nusu fainali baada ya
matokeo ya 3-3 lakini ikinufaika na goli la ugenini. Katika mchezo wa
awali wa nusu fainali, Sevilla iliibuka na ushindi wa 2-0 katika uwanja
wake wa nyumbani, lakini ikapata kipigo cha 3-1 ugenini na kufanya
matokeo kuwa 3-3.
Kwa upande wake Benfica katika mchezo wa kwanza iliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Juventus ya Italia na ugenini ikatoka sare ya kutofungana na wenyeji Juve, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1.
Kwa upande wake Benfica katika mchezo wa kwanza iliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Juventus ya Italia na ugenini ikatoka sare ya kutofungana na wenyeji Juve, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1.
No comments:
Post a Comment