KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, May 2, 2014

Timu tatu za Hispania kucheza fainali za michuano ya vilabu Ulaya, je ni ubora wa soka la Hispania?

 Timu tatu za Hispania zimefanikiwa kucheza fainali mbili tofauti za mashindano yenye hadhi ya juu barani Ulaya mwaka 2014.
Timu hizo mahasimu zimefikia hatua hiyo baada ya Real Madrid kuwachabanga waliokuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo Bayern Munich ya Ujerumani kwa jumla ya mabao 5-0. Real Madrid ilipata ushindi wa bao 1-0 nyumbani, huku ugenini ikiisambaratisha Bayern magoli 4-0.
Nayo Atletico Madrid baada ya kushindwa kuifunga Chelsea katika uwanja wa nyumbani kwa kutoka suluhu ya 0-0, katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali katika uwanja wa Stanford Bridge jijini London, Chelsea ilikiona cha moto kwa kuchabangwa magoli 3-1.
Wachezaji wa Atletico Madrid wakishangilia moja ya magoli yao

Hivyo vita vya ndugu hao Real Madrid na Atletico Madrid vitapiganiwa ugenini katika uwanja wa Estádio do Sport Lisboa e Benfica, ujulikanao pia kama Estádio da Luz (uwanja wa mwangaza)mjini Lisbon, Ureno, Jumamosi tarehe 24 Mei 2014.
Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1967, fainali za kombe la ligi ya mabingwa la UEFA zinafanyika mjini Lisbon.
Baadhi ya wachezaji wa Sevilla walioitoa Valencia

Katika fainali nyingi za kombe la ligi ya Europa, Sevilla ya Hispania inapambana na Benfica ya Ureno mchezo utakaopigwa katika dimba la Turin, nchini Italia Jumatano tarehe 14 Mei 2014.
Sevilla imefuzu kucheza fainali hizo baada ya kuwatoa ndugu zao Valencia katika mchezo wa nusu fainali baada ya matokeo ya 3-3 lakini ikinufaika na goli la ugenini. Katika mchezo wa awali wa nusu fainali, Sevilla iliibuka na ushindi wa 2-0 katika uwanja wake wa nyumbani, lakini ikapata kipigo cha 3-1 ugenini na kufanya matokeo kuwa 3-3.
Kwa upande wake Benfica katika mchezo wa kwanza iliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Juventus ya Italia na ugenini ikatoka sare ya kutofungana na wenyeji Juve, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment