KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, March 27, 2012

Bosi wa Benfica Jorge Jesus amedhamiria kumnyamazisha Didier Drogba


CHAMPIONS LEAGUE
Venue: Estadio da luz
Bosi wa Benfica Jorge Jesus ametamba kujibu tambo za mshambuliaji wa Chelsea Didier Drogba kwa kuwachapa Chelsea mjini katika mchezo wa ligi ya mabingwa usiku huu mjini Lisbon.
Jesus amekubaliana na mshambuliaji huyo lakini akisema pengine alikuwa akitania na kusema anachojua ni kile anachofikiri.
Ananukuliwa akisema
"kwa kile kitakachotokea itakuwa ni kujibu aliyosema na kitaelekea kwa Drogba na kudhihirisha kuwa sisi ni bora kuliko yeye"
Alichokisema Drogba kupitia video ni kwamba wanachokitazama ni kwenye nusu fainali ngumu dhidi ya mabingwa watetezi Barcelona na kusahau msemo wa Kiswahili kuwa usitukane mamba kabwa hujavuka mto.
Sasa Jorge jesus anajibu kauli ya mshambuliaji huyo
Hii maana yake Drogba anaitazama Barcelona kwa kuwa Barcelona are a very, very big team.
Amesahau kuwa timu yake ya Chelsea inajua kuwa Benfica ilivyopanda milima na kuvuka mabonde kufikia hatua hiyo
Chelsea in the Champions League
•2010-11: Lost 3-1 to Manchester United in QF
•2009-10: Lost 3-1 to Inter Milan in last 16
•2008-09: Lost on away goals to Barcelona in SF
•2007-08: Lost on penalties to Manchester United in final
•2006-07: Lost on penalties to Liverpool in SF
Bosi wa Chelsea Roberto di Matteo imejitete kuwa wanakiwango cha ubora cha kutosha licha ya kuwa katika hali mbaya kimatokeo msimu huu.
Kiungo wa Chelsea Frank Lampard anasema wachezaji hawakuwa vizuri kama ilivyotokea wiki iliyopita.
Branislav Ivanovic amesafiri kuelekea Lisbon licha ya kukosekana katika mchezo wa sare ya bila magoli katika ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Tottenham kufuatia kuwa na maumivu.
Kiungo wa kati wa Benfica Luisao anatarajiwa kuwapo kikosini na akitarajiwa kutengeneza “partnership” na  Jardel wakati ambapo mlinzi Ezequiel Garay akiwa katika hatihati ya kuwepo katika mchezo wa leo.
Mfungaji mahiri (Top-scorer) Oscar Cardozo na Rodrigo wanatarajiwa kuongoza sehemu ya ushambuliaji kwa wenyeji usiku huu.
 
Apoel Nicosia v Real Madrid
Kiungo wa Apoel Nicosia raia wa Brazilian Gustavo Manduca anatarajiwa kutokuwepo dimbani hii  leo katika mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya vinara wa ligi kuu ya nchini Hispania Real Madrid baada ya kuondoshwa katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi.
Badala yake kocha Ivan Jovanovic atafanya uchaguzi mwingine .
Madrid itakuwa dimbani bila ya Lassana Diarra, Angel di Maria, Jose Callejon na Ricardo Carvalho wote wakiwa ni majeruhi.
Kiungo Xabi Alonso amesimama kwa adhabu lakini Mesut Ozil kiungo mchezeshaji anarejea baada ya kibano cha kutumikia adhabu ya mchezo wa hivi karibuni dhidi ya Real Sociedad.
Jovanovic anasema changamoto iliyopo ni kwa mabingwa hao mara tisa Madrid hii katika robi fainali kuonyesha uwezo wao mpaka mwisho.
Mpaka kufikia hapo  Apoel ilikuwa katika kundi lililokuwa na timu kama FC Porto, Shakhtar Donetsk na  Zenit St Petersburg na katika hatua ya 16 bora iliindosha timu ya Lyon.
Ananukuliwa Jovanovic akisema
"sisi ni timu ndogo ulaya lakini tuna moyo mkubwa " .
 Bolton kujiapanga White Hart Lane




Bosi wa Bolton Owen Coyle amesema hajua ni jinsi gani vijana wake watafanya kuelekea katika mchezo wa hii leo marudiano wa michuano ya FA katika dimba la White Hart Lane.
Kikosi cha Coyle kitakuwa na kazi kubwa ya kukutana dhidi ya Tottenham mchezo uliopangwa upya baada ya kuvunjika kufuatia  Fabrice Muamba kuzimia ghafla uwanjani March 17.
Ananukuliwa akisema
"tutafanya kile kinacho takiwa kwa kadri ya uwezo wetu kama tunavyofanya mara zote .
Kauli yake pia inakuja wakati huu ambapo hali ya afya ya Muamba ikiimarika.
Anaendelea kunukuliwa akisema
"lakini siwezi kusema itakuwaje mpaka tutakapo kuwa pale uwanjani."
Muamba anaendelea kuimarika kiafya huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 sasa akiweza kutoka kitandani na kuanza kula.
 Anasema
 “Because Fabrice anaendelea vizuri nah ii inaturuhusu sisi kucheza mchezo huu”

Inter Milan imemfukuza kazi Claudio Ranieri baada ya matokeo mabaya

Inter Milan imemfukuza kazi kocha wake Claudio Ranieri baada ya kuwa na matokeo mabaya katika ligi akiwa ameshinda mchezo mmoja katika michezo kumi iliyopita ya ligi kuu ya nchini Italia maarufu kama Serie A.
Bosi huyo wa zamani wa Chelsea alianza kazi San Siro mwezi September akichukua nafasi ya Gian Piero Gasperini baada ya kuwa kazini kama incherge wa benchi la ufundi kwa michezo mitano tu.
Wataalamu wa mambo ya soka nchini Italia wanasema
"inashangaza kwa kuwa kila mtu alijua kuwa angeendelea mpaka kumalizika kwa msimu . Alionekana kama ni mtu ambaye pengine angewabana wachezaji wakongwe lakini inaonekana msimu unazidi kusonga mbele na wachezaji hao wakongwe wanaendelea kupata nafuu ya uwepo wake.
Laurent Blanc na Andre Villas-Boas wanatazamwa kumrithi nafasi yake.

Jana Rais wa klabu Massimo Moratti alinukuliwa akisema  "I think that Claudio Ranieri will remain until the end of the season."lakini sasa mambo yenda tofauti
Kwasasa kocha wa vijana Andrea Stramaccioni anakuwa katika benchi la Inter maarufu kama Nerazzurri.
Stramaccioni anasifa ya kuongoza kikosi cha vijana wadogo wa  Inter ambao walitwaa taji la NextGen mbele ya vijana wa Ajax jumapili iliyopita.
Baada ya kipigo cha jumapili toka kwa Juventus, Inter imekalia nafasi ya nane katika  Serie A, points 22 nyuma ya wapinzani wao wakubwa ambao wanaongoza ligi hiyo.
Mapema mwezi huu waliondoshwa katika hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa na Marseille earlier this month.
Manchester United juu!
Mshambulizi Wayne Rooney alihakikisha timu yake Manchester United inapanda kileleni mwa ligi kuu ya Uingereza kwa kuichapa Fulham bao moja bila.
Bao hilo lilifungwa katika dakika ya 29 ya kipindi cha kwanza pale Rooney alipopokea pasi safi kutoka kwa Jonny Evans.
Kwa ushindi huo sasa Mashetani wekundi wameipiku Man City kwa alama tatu.
Kufikia sasa timu zote zimecheza mechi 30 kila mmoja.
Manchester City sasa wanakibarua kigumu cha kuziba pengo la alama tatu kwani siku ya jumamosi tarehe 31 wataikaribisha Sunderland.
Vijana hao wa Roberto Mancini itawabidi waombe sana Man U wapoteze mechi yao ya siku ya Jumatatu ijayo tarehe 2 April watakapo watembelea Blackburn.
Hata hivyo mkufunzi wa Fulham Martin Jol amelalama kuwa walinyimwa mkwaju wa penalti.
Hii ni baada da ya Michael Carrick wa Manchester United kuonekana kumuangusha mshambulizi Danny Murphy katika eneo la hatari katika dakika ya 87.
meneja huyo wa Fulham amenukulikwa akisema kuwa kila mtu aliyeshuhudia mechi hiyo alitarajia wapewe penalti.

Ahly "haikufurahia" adhabu ya al-Masry
Klabu ya Al Ahly ya Misri imesema "wameshangazwa na kuhuzunishwa" na uamuzi wa kuifungia klabu ya al-Masry kucheza ligi kwa miaka miwili.
Vigogo hao wa kandanda wa Cairo wanaamini adhabu hiyo iliyotolewa na Chama cha Kandanda cha Misri siku ya Ijumaa ingekuwa kubwa zaidi ya hiyo.
Mashabiki 74 walikufa mjini Port Said wakati al-Masry ilipoikaribisha Al Ahly tarehe 1 mwezi wa Februari.
"Tumehuzunishwa na kwa kweli tumekasirishwa," mjumbe wa bodi ya Al Ahly Khaled Mortagy aliiambia BBC.
"Tunaamini haki haikutendeka, inapotokea mashabiki 74 wamekufa katika uwanja wa nyumbani wa klabu hii na bado hii ndio adhabu wanayopewa, ni mwaka mmoja tu wanafungiwa kucheza."
"Kwa sababu, kinadharia, msimu huu umemalizika, kwa hiyo wanaposema wanafungiwa miaka miwili, maana yake halisi ni mwaka mmoja tu."
Wakati msimu wa sasa wa ligi ya Misri ukiwa umefutwa tangu kulipotea ghasia za Port Said, al-Masry wataanza kucheza tena soka kwa msimu wa 2013/2014 - ikiwa na maana watakosa msimu wa mwakani tu.
Klabu hiyo ya Port Said pia imefungiwa kuutumia uwanja wake wa nyumbani kwa muda wa miaka mitatu.
Baada ya al-Masry kushinda mabao 3-1 tarehe 1 mwezi wa Februari, mashabiki wake walivamia uwanja na kuwashambulia wachezaji na mashabiki wa Al Ahly.
Wiki iliyopita Mwendesha Mashtaka mkuu wa Misri aliwafungulia mashtaka ya mauaji na uzembe uliosababisha ghasia watu 75.
Mortagy alisema angependa kuona al-Masry ikifungiwa kushiriki Ligi Kuu kwa angalao muda wa miaka mitano, akitolea mfano unaopaswa kufuatwa ilipofungiwa klabu ya Liverpool baada ya mkasa wa Heysel wa mwaka 1985.
Katika tukio hilo, klabu hiyo ya England ilifungiwa kushiriki mashindano ya Ulaya kwa muda wa miaka sita baada ya mashabiki wake kuonesha utovu wa nidhamu uliosababisha vifo vya mashabiki 39, wengi wakiwa wa klabu ya Juventus.
Licha ya Al Ahly kukusudia kukata rufaa kutokana na uamuzi wa Chama cha Kandanda cha Misri, bodi ya klabu hiyo tayari imeshaamua kutocheza mechi yoyote mjini Port Said kwa muda wa miaka mitano ijayo.
Mabingwa hao mara sita wa Afrika, hawakufurahishwa pia na uamuzi wa kuwataka wacheze mechi zao nne katika uwanja usio na watazamaji, baada ya baadhi ya mashabiki wake kufyatua na kurusha miale ya moto, wakati kocha wao Manuel Jose na nahodha Hossam Ghaly pia wamefungiwa mechi nne kwa kuzozana na maafisa.
Andy Roddick amchapa Roger Federer katika Miami Masters
Roger Federer ambaye anarekodi ya kushinda michezo 16 ya michezo ya Miami Masters amefikia mwisho baada ya kuchapwa  7-6 (7-4) 1-6 6-4 na Andy Roddick katika mzunguko wa tatu wa michezo ya Miami Masters.
Baaba ya kichapo hicho amenukuliwa akisema jamaa huyo raia wa uswiz akisema
"nimetota leo “I came out flat today” ,"
“I was a bit tired, I guess."
Nyota namba moja katika mchezo wa tennis Novak Djokovic yeye amefanikiwa kupata nafasi katika round ya nne baada ya ushindi wa 6-3 6-4 dhidi ya mwenzake msebia toka taifa moja Victor Troicki.
Upande wa wanawake nyota namba moja duniani  katika mchezo huo Victoria Azarenka amesonga mbele kuelekea robo fainali baada ya kumchapa mwanadada toka Slovakia Dominika Cibulkova 1-6 7-6 (9-7) 7-5.

Wladimir Klitschko anajipanga kutete taji
Bingwa wa uzito wa juu katika masumbwi Wladimir Klitschko anatarajiwa kutete taji lake la 12 katika mchezo wa marudiano dhidi ya Tony Thompson mchezo ambao umepangwa kufanyika  July 7 baada ya mpango huo kuwekwa mezani jana na huku mshauri wa , Klitschko Shelly Finkel akiongea na vyombo vya habari.
Hili litakuwa ni pambano la kama kulipiza kisasi.

No comments:

Post a Comment