Harry Redknapp |
Bosi wa
zamani wa Tottenham Harry Redknapp anaamini timu ya taifa ya Uingereza ‘Three
Lions’ lazima ijenge imani kwa vijana ili iweze kuboreka na mabadiliko ya
makocha yanapaswa kutazama vizazi vipya.
Redknapp anaamini
England lazima endeleze vijana ili ifanikiwe katika ngazi ya kimataifa baada
kuondoshwa katika fainali za Euro 2012 na Italia kwa njia ya penati.
Uingereza
imeondoshwa kwa njia ya penati baada ya kuelemewa katika sehemu kubwa ya mchezo
wa jana ndani ya dakika 120 na Italia maarufu kama Azzurri.
Bosi huyo wa
zamani wa Tottenham Hotspur anadhani chama cha soka cha Uingereza FA lazima
iaangalie kizazi kipya ambao wataweza kucheza aina nyingine ya soka.
Akizungumza
na The Sun amesema
"tuwalete
watoto wetu wacheze wacheze. Kubali si suala la nguvu , ukubwa au haraka"
"nina
matumaini makubwa na kituo kipya cha maendeleo
cha St George’s na makocha katika kila hatua nchini Uingereza.
Katika
kampeni yao ya kufuzu kombe la dunia 2014 Uingereza itakuwa na safari kuifuata Moldova
September 7.
No comments:
Post a Comment