Mahasimu
wakubwa katika soka la nchini Hispania watakutana kwa mara ya kwanza katika ule
mchezo maarufu na mkubwa nchini Hispania ndani ya kipindi cha miezi miwili
tangu kuanza kwa msimu mpya wa ligi hiyo katika mchezo wa kwanza utakao pigwa
Camp Nou wakati ambapo mchezo wa marudiano ukipangwa kuchezwa mwezi March
mwakani.
Ratiba ya
ligi kuu ya Hispania maarufu kama La liga imetangazwa ikiwa ni matayarisho ya
msimu mpya wa 2012-13 ambapo macho na
masikio yakiwa yameelekezwa katika mchezo wa mahasimu na wapinzani wakubwa Real
Madrid na Barcelona.
Blaugrana watakutana
na Los Blancos October 7 na mchezo wa marudiano ukipangwa kufanyika Santiago
Bernabeu March 3.
msimu huu
mpya wa ligi ya Hispania unatarajiwa kumalizika August 18.
No comments:
Post a Comment