KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, November 13, 2012

Derby ya Gor Mahia dhidi ya AFC Leopards sasa Jumamosi na Licha ya kuendelea kusugua benchi Balotelli hana mpango wa kuiacha Manchester City. .



Shirikisho la soka nchini Kenya (FKF) limeamua kurudisha nyuma pambano la watani wa jadi katika soka la nchini Kenya baina ya Gor Mahia na AFC Leopards pambano ambalo ni la michuano ya FKF ambapo sasa pambano hilo litapigwa Jumamosi badala ya jumapili.

Katika mkutano uliohudhuriwa na maafisa wa vilabu vyote viwili Gor Mahia na AFC Leopards na kusimamiwa na Rais wa FA Sam Nyamweya kimsingi wamekubaliano mchezo huo upigwe jumamosi katika dimba la Kasarani.

Huo ni mchezo wa nusu fainali ambapo nusu fainali nyingine itakuwa ni kati ya Sofapaka dhidi ya mabingwa wapya wa taji la ligi kuu nchini humo Tusker FC, mchezo ambao utapigwa jumapili huko City Stadium.
       
Licha ya kuendelea kusugua benchi Balotelli hana mpango wa kuiacha Manchester City.
Wakala wa mshambuliaji Mario Balotelli, Mino Raiola amekaririwa akisema kuwa mshambuliaji huyo hana nia ya kuihama klabu yake ya Manchester City, licha ya kuwepo taarifa kuwa mshambuliaji huyo amekuwa akisaka timu ambayo atapata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza

Maneno hayo ya wakala huyo yanafuatia baada ya mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Italia kutokuwepo katika kikosi kilichocheza dhidi ya Tottenham jumapili ambapo pia hakuwepo hata katika orodha ya wachezaji wa akiba.

Katika wiki za hivi karibuni Sergio Aguero na Carlos Tevez wamekuwa wakiwakilisha kikosi cha meneja Roberto Mancini wakati ambapo Edin Dzeko amekuwa akiingizwa akitokea katika benchi.
Raiola anasema
"Baloteli hana mpango wa kuondoka"

DECO :Neymar ni kundi moja na akina Messi na Ronaldo.
Kiungo wa zamani wa Barcelona Deco amewapongeza washambuliaji Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, lakini pia anadhani pia mshambuliaji wa Santos Neymar anastahili kuwemo katika kundi moja na washambuliaji hao.

No comments:

Post a Comment