KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, November 13, 2012

HARAMBEE STARS KUMKOSA WANYAMA NA ORIG OTIENO DHIDI YA TAIFA STARS KESHO.


Kiungo wa kimataifa wa Kenya na Celtic ya Scoitland Victor Wanyama ameshindwa kuja nchini Tanzania na kikosi cha timu yake ya Taifa ya Kenya Harambee Stars kutokana na kile kilichoelezwa kuwa Shirikisho la soka la Kenya Kushindwa kutimiza masharti yake.

Wanyama hapo kabla aliitaka FKF kumrudishia fidia ya nauli yake ya kurudia nchini Scotland ambapo inaarifiwa kuwa ilikuwa ni shilingi za Kenya laki 325,000 (USD 3,200) ambazo zilitokana na mchezo wa oktoba 16 ambapo Wanyama alirejea nchini Kenya kwa ajili ya mchezo wa Harambee Stars dhidi ya Afrika kusini FKF.

Fedha hizo hazikuweza kurejeshwa jambo ambalo halijatekelezwa mpaka leo.

Imeelezwa kuwa familia ya Wanyama imepinga kitendo kama hicho kujirudia wakitaka kwanza kuhakikishiwa juu ya fedha hizo ambapo FKF imetaka kuzirejesha baada ya mchezo na Tanzania.
Amenukuliwa mama yake Wanyama Mildred Ayiemba aking’aka
"hii FA ya Kenya inacheza na mwanagu" 

"Victor alipowauliza juu ya pesa yake maafisa wa FA walikuwa wanamzungusha wachezaji wote wanapewa tiketi za kurudia kwanini hivyo kwa mwanangu?"


Harambee Stars iliwasili jijini Mwanza tangu jana usiku majira ya saa nne bila ya wachezaji wake wawili tegemeo Victor Wanyama na Arnold Orig Otieno huku FKF ikishindwa kuieleza TFF sababu za wachezaji kutokufika.

Wachezaji walio wasili ni pamoja na  Dennis Oliech, Ayub Timbe Masika, Brian Mandela Onyango (Santos), Patrick Oboya, Mzee Patrick Ooko Osiako, Jerry Santo, Fredrick Jerim Onyango Oduor, Edwin Simiyu Wafula (AFC Leopards) na Eugene Ambuchi Asike (Sofapaka).

Wengine ni Geofrey Kokoyo Odhiambo, Mulinge Ndeto, Christopher Wekesa Nyangweso, James Wakhungu Situma (Sofapaka), Peter Odhiambo Opiyo, Charles Elphas Okwemba,  Francis Kahata Wambura (Thika United), Andrew Kiriro Tololwa, Osborne Monday (Sofapaka), Wesley Kemboi na Moses Arita.

Viongozi ni kocha Henry Louis Michel akisaidiwa na Mohammed Ajam Boujarari, Florent Louis Robert Motta, Sunil Shah, Wycliff Obiero Makanga, Wilberforce Bruce Juma, Benson Kennedy Otieno, Ali Abdallah Rehan, Robert Asembo Akumu na Angeline Mwikali Nzavi.


No comments:

Post a Comment