KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, November 10, 2012

Ferguson anasema msimlinganishe Van Persie na Ruud van Nistelrooy hii ni mashine nyingine. Atoa utofauti wao. Chelsea sitaki nataka kwa Cole.

Sir Alex Ferguson amesisitiza kuwa Manchester United haimtegemei sana Robin van Persie ambaye kwasasa yuko katika kizuri.

Van Persie aliyejiunga na United akitokea Arsenal majira ya kiangazi alianza maisha yake mapya katika viunga vya  Old Trafford kwa kung’ara baada ya kufunga mabao 11 katika jumla ya michezo 14.

Mholanzi huyo ambaye alianzia benchi katika mchezo dhidi ya Braga mchezo wa vilabu bingwa ulaya alidhihirisha ubora wake baada ya kuingizwa dimbani kwa kufunga goli la pili zuri na hivyo maswali kuanza kuibuka juu ya uwezo wa United kucheza bila ya yeye.

Vijana wa mzee Ferguson sasa wamekuwa wafunga magoli katika kila mchezo ambapo mshambuliaji huyo gumzo nchini England na duniani kwa ujumla akiwa ni miongoni mwa wafumania nyavu wa juu katika ligi ya England na ligi ya mabingwa ulaya.

"sidhani kama ni tatizo kumtegemea Robin, mwaka jana tulipoteza taji kwa tofauti ya bao la kufunga na kufungwa . sitaki kupoteza tena taji kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa"
Van Persie tangu ajiunge na United amekuwa akiwakumbusha mashabiki wa United enzi za Ruud van Nistelrooy jambo ambalo hata hivyol Ferguson hapindezwi nalo.

"Robin ni mchezaji tofauti na van Nistelrooy,"
"Ruud alikuwa ni mshambuliaji wa ndani ya kisanduku cha hatari lakini . Robin yuko katika utofauti katika kuelewa mchezo"

"hatukudhani kama tungempata. Kulikuwa na dhana kuwa huenda Arsenal ingefanikiwa kumbakisha Emirate"

 Lakini alipoamua kundoka tulipata nguvu mpya kwa kwa kweli ni miongoni mwa wachezaji bora katika biashara ya soka."
Leo United watakuwa dimbani dhidi ya Aston Villa.

Chelsea hawako tayari kumuachia Cole aondoke.
Klabu ya Chelsea imesema kuwa haiko tayari kumuachia  mlinzi wake wa pembeni Ashley Cole aondoke na kujiunga na Paris Saint-Germain au hata klabu nyingine kubwa barani Ulaya mnamo mwezi Januari.

Mabingwa hao wa soka wa vilabu barani Ulaya wamethibitisha juu ya kuendelea kuwepo kwa mazungumzo baina yao na mwakilishi wa Cole na kwamba huenda wakafikia tamati kabla ya sikukuu ya Christmas katika kujaribu kumzuia mlinzi huyo na huenda akasaini mkataba mpya.

Meneja wa klabu hiyo Roberto Di Matteo na viongozi wengine waandamizi wa klabu hiyo wamekuwa wakimtaka mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich kuachana na mpango wake wa kuwaacha wachezaji wenye umri zaidi ya miaka 30 na kumuongezea Cole mwaka mmoja baada ya mkataba wake kumalizika.

No comments:

Post a Comment