KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, December 27, 2012

ROBERTO MANCINI AKIRI KUVURUNDA NA KUSEMA KAZI IPO MSIMU HUU.

Kocha wa Manchester City Roberto Mancini.
Kocha wa Manchester City, Roberto Mancini, amesema klabu hiyo inakabiliwa na tatizo kubwa kufuatia kushindwa kwa bao moja kwa bila na Sunderland.

Mabingwa hao watetezi, walipoteza nafasi nyingi za kufunga wakati wa mechi hiyo, na kupoteza alama tatu muhimu, hatua inayowaweka alama saba nyumba ya vinara wa sasa Manchester United.

Man City imefunga magoli 34 baada ya kucheza mechi 19, katika mechi za ligi kuu msimu huu, idadi ambayo ni magoli kumi na nne chini ya magoli waliyofunga mahasimu wao Manchester United ambao waliilaza Newcastle 4-3 siku ya Jumatano.

Zaidi ya yote Man City imefunga magoli 12 kwa mechi tisa za ugenini ukilinganisha na United ambayo imefunga magoli 22 kutoka kwa mechi 10.

No comments:

Post a Comment