Stewart Downing. |
Winga huyo
alikuwa akihangaika katika kipindi kirefu tangu ajiunge na klabu hiyo majira ya
kiangazi mwaka 2011 kwa ada ya uhamisho wa pauni milioni 20 jambo ambalo
lilipelekea Liverpool kutaka kumuuza mwezi Januari lakini sasa
mwingireza huyo amefanikiwa kuimarisha kiwango chake na sasa atasalia Anfield.
Amekaririwa
meneja Liverpool Brendan Rogers akisema
"ndani
ya kipindi cha wiki sita mpaka saba uwezo wake umeimarika na amekuwa akicheza
katika nafasi mbalimbali, nilifurahishwa naye alipokuwa dimbani katika mchezo
dhidi ya Fulham jumamosi.
Alifunga goli , alitengeneza goli na alikuwa sawasawa.
Alicheza pia vizuri dhidi ya Aston Villa katika eneo la ulinzi wa pembeni.
Uchezaji wa Downing
umemvutia Rodgers kiasi kuelezea kuwa anataka mchezaji huyo asalie Anfield kwa
kipindi kirefu zaidi.
Te Klose ameazimwa kuwa mkurugenzi wa
michezo wa Chivas de Guadalajara.
Kikosi cha Chivas. |
Dennis Te
Klose anakuwa Rais mpya wa shughuli za uendeshaji michezo katika klabu ya Chivas
na Chivas USA,klabu ya Guadalajara imetangaza hapo jana.
Mduchi huyo
ana uzoefu wa miaka 10 katika masuala ya soka nchini Mexico, ambapo pia aliwahi
kuwa mkurugenzi wa michezo wa Chivas USA katika kipindi kifupi wakati huo klabu
hiyo ikianza shughuli zake za uendeshaji wa klabu. Alianza kazi katika soka
kama mtafuta wachezaji wa Chivas.
Te Klose kwa
kipindi kirefu pia amefanya kazi kama mkurugenzi wa soka la vijana katika
shirikisho la soka la nchini Mexico. Alisifika kama mtu mwenye uwezo wakuona
vizuri na kutambua vipaji katika shirikisho la soka la Mexico na vilabu vya
vijana huko Tigres.
Steven Gerrard kuongezwa mkataba Liverpool.
Meneja wa Liverpool
Brendan Rodgers anataka kumuongezea mkataba kiungo Steven Gerrard akisema
kiungo huyo bado ana mengi yakutoa katika uchezaji wake.
Mkataba wa
sasa wa Gerrard Anfield unatarajiwa kumalizika kuelekea kumalizika kwa msimu wa
2013/2014.
Kiungo huyo
wa kimataifa wa England amefunga jumla ya mabao 153 katika michezo
aliyoitumukia Liverpool.
Amenukuliwa kupitia
mtandao wa klabu Rodger akisema
"si
dhani kama kuna swali lolote, tunataka kumuongezea mkataba".
Gerrard alianza
kuitumikia Liverpool mwaka 1998 na kuiongoza klabu hiyo kama nahodha katika
kipindi cha mafanikio cha kuchukua taji la ubingwa wa vilabu Ulaya mwaka 2004-05.
Akiwa na Liverpool
ametwa mataji mawili ya FA na, League Cup mata tatu pamoja na taji la Uefa Cup.
Zubizarreta: Barca haita muuza David
Villa.
Mkurugenzi wa
soka wa Barcelona Andoni Zubizarreta amesisitiza kuwa amesema Arsenal iachane
na wazo la kumununua David Villa mwezi Januari kwani mchezaji huyo hawatamuuza
kwa kuwa klabu hiyo haina utaratibu wa kuwauza wachezaji wake muhimu katika
kipindi cha nusu msimu.
Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa katika vita kubwa ya kusaka nafasi ya
kucheza katika kikosi cha kwanza hasa mara baada ya kufanikiwa kuponya maumivu
ya mguu yaliyokuwa yakimsumbua ambapo sasa inaarifiwa huenda akaondoka Barca
mwezi January.
Arsenal imekuwa
ikitajwa kuwa ikimtaka Villa lakini Barca wanasema hakuna mpango wowote wa
uhamisho utakao fanyika mwezi January.
Amenukuliwa Zubizarreta
na Canal Plus akisema
"mwezi
januari tutaendelea kusalia na Villa na ni muhimu kukumbuka kuwa ni klabu ina
tabia ya kukataa ofa za za mwezi huo, David ni mchezaji ambaye analeta magoli
na uzuri wa kikosi
"sasa
amerejea kutoka katika maumivu makali naamini kuwa anaendelea kuwa katika
kiwango bora uwanjani licha ya kwamba ni kawaida kwa mchezaji mkubwa yoyte huwa
anasaka nafasi ya kucheza na hilo ni zuri kwa ushindani wa kweli ndani ya
kikosi"
No comments:
Post a Comment