KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, January 14, 2013

GOLIKIPA WA KIHISTORIA WA MAREKANI KESEY KELLER NA MLINZI WA PEMBENI WA SEATTLE SOUNDERS BURCH WAFANYA KLINIKI SHULE ALIYOSOMA MBWANA SAMATTA NA MOHAMED SAMATTA YA MBAGALA MCHIKICHINI NA KUTOA FULANA NA VIFAA VYA MICHEZO JIONI WASHUHUDIA PAMBANO LA SIMBA B NA AFRIKAN LYON B UWANJA WA KARUME.

Rahim zamunda mkurugenzi wa klabu ya Afrikan Lyon akiwa na wageni wake mlinda  mlango wa zamani wa kimataifa wa Marekani wa Kasey Keller na Marc Burch katika shule ya Mbagala mchikichini alikosoma Mbwana Samata wa TP Mazembe na na mdogo wake Mohamed Samata wa Afrikan Lyon.
Mohamed Samata wa Afrikan Lyon akiwakaribiza wachezaji wa Keller na Marc Burch katika shule aliyosoma yeye na mdogo wake Mbwana.
Wanafunzi wa shule ya msingi MbagalaMchikichini.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mchikichini wakimsiliza Rahim Zamunda akiwapa maelekezo.
Mlinda mlango Kasey Keller akivaa buti kabla ya kuanza kucheza soka na wanafunzi wa Mchikichini.
Marc Burch mlinzi wa Seattle Sounders akifurahia Klinic na wanafunzi wa Mchikichini.
Rahim naye kumbe wamo.
Kasey Keller na Marc Burch wakiwa na Mohamed Samata katika picha ya pamoja na wanafunzi.

 JIONI WAKIWA UWANJA WA KARUME.

Kasey Keller awaambia wachezaji wa timu za B kuongeza juhudi katika soka kwani yeye alianza akiwa kijana na alifanikiwa hivyo waiige mfano wake na wasikate tamaa, pembeni yake ni Goefrey Nyange Kaburu.
Huu ulikuwa ni mchezo wa Afrikan Lyon B dhidi ya Simba B ambao ulihudhuriwa na Keller na Burch uiimalizika kwa suluhu ya 0-0 uwanja wa Karume.
Keller amekuwa mlinda mlango namba moja wa timu ya taifa ya Marekani mara nne katika fainali za kombe la dunia na mmoja wa walinda mlango wa kwanza kuwa namba moja katika vilabu vya ligi kuu ya nchini England.

Katika miaka ya 1997,1999 na 2005 alitajwa kuwa mwanamichezo bora wa mwaka ikiwa ni nadra kupata tuzo kama hiyo mara.

Mzaliwa huyo wa kitongoji cha Olympia, Keller amecheza zaidi ya mechi katika ngazi ya klabu na timu ya taifa. Amekuwa mlinda mlango mwenye rekodi kubwa zaidi ya kuidakia timu ya taifa ya Marekani akidaka michezo 102 na kushinda michezo 53 kati ya hiyo.

Ameshiriki kombe la dunia mara nne, ambapo mwaka 1996 alikuwa nahodha wa timu ya taifa ya nchi hiyo iliyoshiriki michezo ya Olympic.

Alijiunga na Millwall ya England na kuanza kucheza soka la kulipwa la kueleweka kwa mara ya kwanza katika ligi ya daraja la kwanza hiyo ilikuwa May 2, 1992 kabla ya kuelekea Leicester City miaka minne baadaye wakati huo ikishiriki ligi kuu ya England ‘Premier League’ ambapo mwaka 1997 walishinda taji la ‘League Cup’.

Baada ya misimu mitatu na Leicester City alijiunga na Rayo Vallecano iliyokuwa ikishiriki ligi kuu ya Hispania ‘La Liga’. Baadaye alirejea Premier League ambapo alijunga na Tottenham Hotspur katika misimu miwili ya 2002-03 na 2003-04. 

January 15, 2005, Keller alijiunga na Borussia Mönchengladbach ya Ujerumani kabla kuondoka huko na kurejea kwa mara ya tatu Premier League ambapo alijiunga na klabu ya jijini London katika viunga vya Craven Cotage na Fulham.

Kwa upande wake Marc Burch mzaliwa wa Cincinati, Ohio hana historia ya kutisha ambapo alianzia soka chuo kikuu cha Maryland kabla ya kuelekea D.C. United mwaka 2007 mpaka 2011 na baadaye akajiunga na L.A. Galaxy mwaka 2006 kabla ya kuelekea Columbus Crew na baadaye mwaka jana akajiunga Seattle Sounders ambayo anaichezea mpaka sasa.
Huo ndio ugeni wa kisoka ulioko hapa nchini.

No comments:

Post a Comment