KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, January 24, 2013

HABARI ZA KIMATAIFA: Rais wa AC Milan Berlusconi anadai hana mpango na Balotelli wala Kaka na Sneijder na mkewe Yolanthe wanasema wanajisikia kama wako nyumbani nchini Uturuki.


  Rais wa AC Milan Silvio Berlusconi amesema kuwa klabu yake haina mpango wa kumchukua mshambuliaji wa Manchester City Mario Balotelli wala kiungo wa Real Madrid Ricaldo Kaka.
Kauli yake hiyo inazima uvumi ulikuwepo kuwa walikuwa kwenye mpango wa kumchukua Balotelli ambaye amekuwa katika sintofanhamu ndani ya klabu yake na kwamba walikuwa tayari kutoa pauni milioni £20 zikiwa ni taarifa za ndani.

Mialn pia ilikuwa ikihusishwa kuwepo katika mazungumzo na Real Madrid juu ya uwezekano wa kumrejesha Kaka San Siro, habari ambazo Berlusconi maezikanusha kwa madai ya kwamba kwa sasa hawana fedha ya kufanya uhamisho wa aina yoyote.

Akiongea na Radio 2 ya nchini Italia, Berlusconi amekaririwa akisema

"Si Balotelli wala Kaka atakayekuja Milan. Hizi ni dili zisizowezekana katika kipindi hiki."

 Sneijder: Najisikia kama niko nyumbani ndani ya Uturuki.
 Wesley Sneijder ametanabaisha kuwa anajisikia kama yuko nyumbani akiwa nchini Uturuki.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Uholanzi amejiunga na Galatasaray akitokea Inter Milan mapema wiki hii kwa ada ya euro €7.5 huku akisema amefarijika kuanza kazi katika timu yake mpya.

Akiongea na Galatasaray TV Sneijder amesema

"Huu ni ujumbe kwa ukaribisho wa aina yake kuwahi kutokea hapa Such an amazing welcome message could only be seen here, mke wangu Yolanthe ameniambia kuwa nimefanya maamuzi sahihi'.

"Tangu tulipowasili tunajisikia kama tuko nyumbani na hili ndio jambo la muhimu, najisikia raha kuwepo hapa"

No comments:

Post a Comment