KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, January 18, 2013

LIVERPOOL WAKO KATIKA MPANGO WA KUMNASA SNEIJDER.

 Barely played: Wesley Sneijder has been frozen out at Inter Milan
Liverpool itaingia katika mbio za kumnasa Wesley Sneijder endapo kiungo huyo wa kimataifa wa Uholanzi atakubali kupunguza mahitaji yake makubwa ya mshahara anayotaka kwasasa.
ingawa Sneijder anaonekana hafanani na sifa za aina ya wachezaji ambao wamiliki wa Liverpool wa FSG wamekuwa wakiwalenga ambazo ni umri mkubwa wa miaka 28 na gharama ya mshahara wa pauni milioni 6 kwa mwaka lakini meneja wa klabu hiyo Brendan Rodgers ameonekana kumtamani kiungo huyo nguli.
Galatasary ndio klabu pekee kuonyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo wa Inter Milan na sasa wanataka majibu ya mpango wa mchezaji huyo hii leo.
Sneijder anaonekana kuwa na wasiwasi juu ya kuelekea Uturuki na anadhani kuna haja ya kucheza soka karibu na nyumbani Uholanzi kutokana na sababu za kifamilia.
Inter italazimika kuachia aondoke kwa pauni milioni £6.2 lakini kuelekea Anfield itategemea na punguzo la mshahara uliotakiwa na Sneijder mwenyewe. 
Sneijder anafahamu kuwa masiha yake ya soka katika klabu ya Milan yanafikia mwisho mwezi huu lakini juu ya hatma yake ya baadaye amenukuliwa akisema.
Na hapa amenukuliwa na Gazzetta dello Sport akisema
'Tazama wachezaji wote ambao wako katika soko la uhamisho katika soko la wachezaji kipindi hiki wanaaamua nini cha kufanya kabla ya January 31, na mimi nitafanya hivyo o,'.
'sitaki kuharakisha na vilevile sitaki kuharakishwa.
Not a question of money: Sneijder claims wages are not the issue
'baada ya kila kitu kuwa kimekamilika sitaki kuwa katika fikra hizo za kulazimishwa kuchagua jambo la kimaisha.'

No comments:

Post a Comment