KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, January 7, 2013

YANGA KUDHIHIRISHA UKUBWA WA SOKA YAKE KWA DENIZLISPOR YA DARAJA LA KWANZA UTURUKI BAADA YA KUWASUMBUA BIELEFELD YA UJERUMANI.(Chanzo picha na habari kutoka www.youngafricans.co.tz)

Ernest Brandts akiwa mazoezini asubuhi ya leo kutoka kushoto ni Saidi Bahanuzi, Haruna Niyonzima na Simon Msuva.
Ernest Brandts na Minziro wakiongoza mazoezi asubihi ya leo.
 Klabu bingwa Afrika mashariki na kati Yanga kesho itashuka dimbani kucheza mchezo wake wa pili wa kirafiki wa kujipima nguvu dhidi ya Denizlispor FC inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Uturuki mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Selen Football -Kalimya Complex pembeni kidogo ya mji wa Antlaya.
 
Yanga ambayo imeweka kambi ya mafunzo jijini Antalya kwa wiki mbili itatumia mchezo huo kama fursa ya kujipima nguvu na timu hiyo la Denizlispor FC  ambayo imeshuka kutoka ligi kuu ya Uturuki mwaka jana na hivi sasa inapamabana kurudi tena katika Ligi Kuu ya Uturuki.
 
Kocha Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema kwao ni furaha kupata nafasi ya kucheza na timu kubwa kama ya Denizlispor FC ambayo ina wachezaji wa kiwango cha kimataifa hivyo anaamini utakua ni mchezo safi na kuwavutia.

Baada ya kuwa na wiki moja ya mazoezi na mechi moja ya kirafiki dhidi ya Armini Bielefeld ya ujerumani mwishoni mwa wiki itakua ni fursa nyingine nzuri ya kucheza mchezo wa kirafiki na timu nyingine, hii itanisadia kuona maendeleo ya kikosi kutokana na mazoezi ambayo wamekuwa wakifanya tangu walipofika Antalya
 
Denizlispor FC ni miongoni mwa timu zaidi ya 200 kutoka sehemu mbalimbali duniani ambazo zimeweka kambi katika mji wa Antlaya kwa ajili ya maandilizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Daraja la kwanza nchini Uturuki.
 
Mchezaji wa zamani wa Leicester City ya Uingereza, Dundee United ya Scotland na Ivernes ya Uholanzi, mtanzania mzaliwa wa Uingereza Eric Odhiambo ni miongoni mwa washambuliaji wa kutegemewa wa timu ya Denizlispor FC. 
 
Young Africans imeendelea na mazoezi katika viwanja wa Fame Residecne tayari kabisa kujiandaa na mchezo huo utakaochezwa kesho katika uwanja wa Selen Football - Kalimya complex pemebeni kidogo ya mji wa Antalya.

Kikosi cha wachezaji 27 waliopo mjini Antalya wote wako katika hali nzuri na hakuna maheruhi hata mmoja hali itakayompa kocha Brandts kuamua kumtumia mchezaji yoyote katika mchezo huo.
 
Athumani Idd 'Chuji' na Hamis Kiiza waliokuwa wakijisikia vibaya kabla ya mchezo wa juzi dhidi ya Amrnini Bielefeld wanaendelea vizuri na wanaendelea na mazoezi pamoja na wachezaji wengine waliopo na timu mjini Antalya. 
 
Kuhusu hali ya hewa leo haijaonekana kuwa tatizo kwa wachezaji kwani wanaonekana kuimudu na muda mwingi kwa sasa kumekua na jua linalowaka kuanzia asubuhu wakati wa mazoezi mpaka mida ya jioni, kwa leo hali ya hewa ni nyuzi joto 17 - 21, hivyo hali ya hewa ni nzuri tu.

No comments:

Post a Comment