KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, January 5, 2013

YANGA KUWAVIMBIA WAJERUMANI LEO

Timu ya Yanga leo itashuka dimbani kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Arminia Bielefeld ya Ujerumani katika mchezo utakaofanyika mjini Antalya majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki na Kati 

Yanga ambayo imeweka kambi ya mafunzo katika mji wa Antalya imekuwa ikifanya mazoezi tangu siku ya jumatatu na wachezaji wote wameonekana kufurahia mazingira ya kambi na huduma zote kwa ujumla.
 
Baada ya kufanya mazoezi kwa takribani siku tano (5) mfiululizo itatumia mchezo wa leo jioni dhidi ya timu ya Arminia Bielefed kama kipimo tosha cha maendeleo ya mafunzo yanayoendelea nchini Uuturuki.
 
Kocha Mkuu wa Young Africans mholanzi Ernie Brandts amesema anashukuru  wachezaji wake wapo fiti kwa ajili ya mchezo kesho, na kwa kuwa hakuna mchezaji majeruhi atakuwa na fursa ya kumtumi amchezaji yoyote katika mechi hiyo.
 
Aidha Brandst amesema kuwa anajua mchezo wa leo utakua mgumu kwani timu ya Arminia Bielefeld ni timu nzuri na imekua ikishiriki ligi kuu ya ujerumani mara kadhaa, hivyo ni timu ambayo itatoa ushindani mkubwa sana

No comments:

Post a Comment