Tony Thompson akimkalisha David Price katika raundi ya pili. |
David Price amehakikishiwa nafasi nyingine ya kulipiza kisasi dhidi ya Tony Thompson baada ya makubaliano kufikiwa kuwa pambano hilo lichezwe Julai 6.
Mpiga ndonga huyo mwenyeji wa Liverpool alitota vibaya katika raundi ya pili tu ya pambano lake la kwanza la kulipwa la uzito wa juu dhidi ya mkali wa ngumi raia wa Marekani Thompson mwezi uliopita.
Endapo Price ataibuka na ushindi mara hii, hiyo itamrejeshea heshima yake katika ulimwengu wa masumbwi hasa nchini Uingereza.
Mwandaaji kijana wa pambano hilo mwenye umri wa miaka 29 Frank Maloney ametanabaisha kuwa pambano hilo litakalo pigwa katika ukumbi wa Echo Arena lilikuwa gumu kuliandaa kwa mara nyingine.
'Kwasababu lilikuwa ni pambano kubwa kwa Thompson kulikuwa kuna mengi yakuvutia kwa mapromota lakini hatimaye tumetia saini.
'Kulikuwa na wachezaji wengi wa kucheza na David lakini yeye na mwalimu wake Franny Smith wameonelea kucheza tena na Thompson.
Price akipokea kipokea konde la mkono wa kulia.
No comments:
Post a Comment