KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, March 28, 2013

HABARI ZA MICHEZO KIMATAIFA : Giggs anaamini wengi watafikia umri wake katika soka. Wilshere huenda akasubiri sana kufuatia maumiu ya kifundo cha mguu.XAVI HERNANDES AOMBA KUWA FITI DHIDI YA PSG . Trancesco Totti anasema baada ya Messi hakuna kama yeye. NA Rooney anasema Engalnd ijifunze kutokana na makosa.

Kiungo wa mashetani wekundu Manchester United Ryan Giggs anaamini anaamini kabisa kuwa inawezekana kwasasa mchezaji kuwa na nguvu ya kucheza soka mpaka katika umri wa miaka ya mwishoni ya thelathini kutegemeana na aina ya mikataba na maendelao ya kiteknolojia.
Giggs aliyeanza kucheza soka katika klabu ya Machester United mwezi mwaka Machi 1991 akiwa na umri wa miaka 17 na sasa ni zaidi ya miaka 22, bado anaonekana ni mwenye nguvu na msimu huu amekamilisha jumla ya michezo elfu moja.
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Wales, tarehe mosi mwezi huu amesaini tena mkataba wa mwaka mmoja na United mkataba ambao utamfanya kuwa ni mchezaji wa tatu kufikia umri wa miaka 40 akiwa kama ilivyokuwa kwa akina Teddy Sheringham na Gordon Strachan, jambo ambalo anaamini ni la kawaida.
Wakati United ikielekea katika michezo miwili migumu dhidi ya Sunderland jumamosi na baadaye katika uwanja wa Stamford Bridge kukabiliana dhidi ya Chelsea mchezo wa robo fainali ya michuano ya FA, Giggs analiangalia jambo hilo la kucheza michezo yote miwli ndani ya kipindi cha siku tatu kwake litakuwa ngumu.

 Wilshere huenda akasubiri sana kufuatia maumiu ya kifundo cha mguu.

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa majeraha yanayomkabili kiungo wake kiungo wake mahiri Jack Wilshere huenda yakamuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu.
Wilshere mwenye umri wa miaka 21 aliondolewa katika kikosi cha timu ya taifa ya England kuelekea katika michezo miwili ya kuwania kufuzu fainali ya kombe la dunia dhidi ya San Marino na Montenegro kufuatia kujitokeza tena kwa maumivu yake ya kifundo cha mguu yaliyopelekea kuwa nje ya uwanja msimu mzima uliopita.
Licha ya vyombo mbalimbali vya habari kuandika juu ya kurejea kwa kiungi huyo katika hali yake ya kawaida katika wiki za hivi karibu, bado Wenger anadai kuwa maumivu hayo huenda yakamuweka nje ya uwanja kwa nyakati tofauti na kwamba kwasasa hajui ni lini atarejea uwanjani.
Meneja huyo mfaransa pia amesema Theo Walcott, Kieran Gibbs na Abou Diaby huenda wakaungana katika benchi na kiungo katika mchezo wao wa jumamosi dhidi ya Reading.

 XAVI HERNANDES AOMBA KUWA FITI DHIDI YA PSG

Kiungo wa Barcelona Xavi Hernandez amesisitiza kuwa atakuwa fiti kimchezo katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Paris Saint-Germain Jumanne.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa na maumivu ya msuli yaliyopelekea kukosa mazoezi ya leo asubuhi ambapo amelazimika kufanyiwa matibabu ya kunyoosha misuli (physiotherapy).
Xavi atalazimika kupumzishwa mchezo wa Jumamosi wa ligi kuu ya nchini Hispania La Liga dhidi ya Celta, huku bado mashaka yakiwepo kuelekea katika mchezo dhidi ya PSG jijini Paris.
Amenukuliwa akisema
"Sitacheza dhidi ya Celta mwishoni mwa juma, lakini nitakuwa tayari dhidi ya Paris Saint-Germain,".
Barca iliwakosa Adriano, Jordi Alba, Carles Puyol na Pedro katika siku za hivi karibuni kufuatia kukabiliwa na majeruhi.

Trancesco Totti anasema baada ya Messi hakuna kama yeye.

Mshambuliaji mkongwe wa Roma Francesco Totti amejisifu kuwa ni mshambuliaji mmoja tu aliye na uwezo zaidi yake katika ulimwengu huu wa soka na huyu si mwingine bali ni Lionel Messi wa Barcelona.
Totti mwenye umri wa miaka 36 ambaye alikuwa akihusishwa na kurejea katika timu ya taifa kufuatia msimu huu kuwa katika kiwango cha juu, amesema kuwa Messi ni kiwango kingine lakini ukiachana na Messi hakuna mwingine zaidi yake.
Akiongea na La Gazzetta dello Sport Totti amesema kuwa duniani kwasasa kuna mchezaji mmoja tu ambaye anafanya vitu ambavyo yeye hawezi kufanya ambaye ni Messi na pia hadhani kama nchini Italia kuna mchezaji kama yeye.
Mshambuliaji huyo mzoefu pia akaenda mbali zaidi akimpongeza kocha Marcello Lippi , huku pia akisema angependelea baadaye kufanya kazi na Jose Mourinho.
Totti amemponda mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli akisema mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City bado si lolote si chochote.

Rooney anasema Engalnd ijifunze kutokana na makosa.

Mshambuliaji wa Manchester United na timu ya taifa ya England -Wayne Rooney anaamini kuwa England itakuwa imejifunza kutoka na makosa yaliyo jitokeza katika mchezo uliomalizika kwa sare dhidi ya bao 1-1 dhidi ya Montenegro.
Kikosi cha kocha Roy Hodgson walikuwa wakiamini kuwa wangeibuka na ushindi katika mchezo huo baada ya bao la mapema la Rooney kunako dakika ya sita ya mchezo lakini wageni wakafaniwa kusawazisha.
Rooney mwenye umri wa miaka 27 anaamini kuwa kuna haja ya kurejea na kujipanga upya kwa ajili ya michezo iliyosalia ya kampeni ya kuwania kufuzu fainali ya kombe la dunia ambapo michezo mitatu kati ya minne iliyobaki italuwa ikichezwa katika uwanja wao wa nyumbani wa Wembley.
Amenukuliwa akisema
"Bado tuna nafasi kubwa ya kufuzu, hilo lilikuwa ni somo kwetu hususani katika kipindi cha pili na tunapaswa kujifunza na kusaka namna ya kufanya vema.

No comments:

Post a Comment