KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, March 15, 2013

KIMATAIFA: Barcelona kukutana na Paris St-Germain robo fainali ya vilabu bingwa Ulaya na Di Canio akanusha safari ya kwenda Madejeski kuhusiana na ajira ya Reading.


 Paolo Di Canio amekanusha kuwa matembezi yake yakutembelea uwanja wa Madejski mwishoni mwa wiki kuwa kuna uhusiano na kuondoka kwa aliyekuwa meneja wa Reading Brian McDermott.
Bosi huyo wa zamani wa Swindon alipigwa picha akiwa katika eneo la wakurugenzi wa klabu ya wakati wa mchezo ambao Reading walifungwa kwa mabao 2-1 na Aston Villa.
Kuonekana kwake katika mchezo huo kulichukuliwa kama ni sehemu ya mchakato wa kuelekea kuchukua nafasi ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo aliyetupiwa virago vyake McDermott.
Di Canio amekaririwa na BBC Sport Di Canio akisema kuwa alikwenda katika mchezi huo kwa lengo ka kuangalia mchezo huo na si vinginevyo.
McDermott meneja wa zamani wa Reading alifukuzwa kazi na Reading Jumanne wiki hii baada ya kupata matokeo mabaya ya kufungwa michezo minne mfululizo ya ligi kuu ya soka nchini England.

Barcelona kukutana na Paris St-Germain robo fainali ya vilabu bingwa Ulaya
Droo ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya imefanyika hii leo ambapo mabingwa mara nne wa taji hilo Barcelona watakuwa wakocheza dhidi ya vinara wa ligi kuu nchini Ufaransa Paris Saint-Germain.
Michezo ya mkondo wa kwanza ya hatua hiyo ya robo fainali inatarajiwa kuchezwa April 2 na 3 kabla ya michezo ya marudiano ambayo itachezwa April 9 na 10.
Kikosi cha Joes Mourinho, Real Madrid chenyewe kitakuwa na kazi dhidi ya timu ya mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba, Galatasaray, wakati ambapo Bayern Munich waliotinga fainali ya msimu uliopita wakikutana dhidi ya Juventus nao Malaga dhidi ya Borussia Dortmund.
Droo hiyo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1996 itakuwa imezikosa timu za nchini England katika hatua hiyo ya michuano.
Paris Saint-Germain itakuwa na nahodha wa zamani wa England David Beckham ambaye atakuwa akionekana katika hatua hiyo ya michuano ya vilabu Ulaya kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1995.
Meneja wa zamani wa Chelsea Jose Mourinho atakuwa na kazi ya kusaka mbinu ya kulinda makali ya mshambuliaji wake wa zamani katika klabu ya Chelsea Didier Drogba wakati kigogo cha Hispania, Real Madrid watakapo kutana dhidi ya klabu mpya ya Drogba, Galatasaray.
Bayern Munich ambao walipoteza katika fainali ya msimu uliopita kwa Chelsea watakuwa na kazi dhidi ya  Juventus ambayo haijapoteza michezo yake ya msimu huu katika michuano hii.
Timu nyingine ambayo haijapoteza mpaka sasa ni Borussia Dortmund ambao ambao watasafiri nchini Hispania kuwafuata Malaga katika mchezo wa mkondo wa kwanza mchezo ambao utakuwa ni kwanza kuwakutanisha katika michuano ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment