KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, March 12, 2013

UKURASA MICHEZO KIMATAIFA: Wilshere kuwakosa Munich na michezo ya kimataifa ya England. Franz Beckenbauer anamtaka Rooney achezee Munich na Gerrard anasaka mafaniko ya kumaliza vema msimu kwa kupata nafasi nne za juu.......

Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere atakuwa nje ya uwanja wa kipindi cha wiki tatu kuanzia sasa, kufuatia kupata maumivu ya kifundo cha mguu na hivyo kupelekea kukosekana katika michezo mingine ya England kuwania kufuzu kombe la dunia dhidi ya San Marino na Montenegro mwezi huu.


Majeraha hayo pia yatamuweka nje kiungo huyo mwenye umri wa miaka 21katika mchezo wa marudiano wa klabu bingwa Ulaya baina ya timu yake ya Arsenal dhidi ya Bayern Munich mchezo ambao umepangwa kufanyika Jumatano.


Arsenal kwasasa iko nyuma ya Munich kimatokeo kwa mabao mabao 3-1 yaliyopatika katika mchezo wa kwanza.
 

Wilshere alikumbwa na maumivu hayo ya kifundo cha mguu wake wa kushoto katika mchezo ambao washika bunduki hao walifungwa kwa mabao 2-1 na Tottenham Machi 3.

Itakumbukwa katika msimu uliopita Wilshere alikosekana katika msimu mzima kufuatia maumivu ya kifundo cha mguu wa kulia.

Licha ya kucheza michezo saba tu katika msimu huu, Wilshere anatazamwa kuwa ni kiungo muhimu katika kikosi cha kocha wa Roy Hodgson wakati huu ambapo England ikiwa katika kampeni ya kufuzu fainali za kombe la dunia 2014 nchini Brazil.


Franz Beckenbauer anamtaka Rooney.

Kigogo kutoka pande za Bavaria, Bayen Munich kinatarajia kukaribisha usajili wa  mshambuliaji wa Manchester United ambaye amekuwa akizungumzwa kama mmoja wa wachezaji bora duniani.

Franz Beckenbauer anasema angependelea Bayern Munich kumsajili Wayne Rooney.

Tetezi nyingi zimezagaa zikihusisha hatma ya baadaye ya mshambuliaji huyo wa Manchester United baada ya kuondolewa katika kikosi cha kwanza cha meneja Alex Ferguson katika mchezo wa pili wa vilabu bingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid.

Franz Beckenbauer mwenye historia ya kuwa nahodha wa Ujerumani mwenye mafanikio makubwa kwa muda mrefu amekuwa aakivutiwa na Rooney, akimuelezea kuwa ni

"mmoja kati ya wachezaji wakubwa sana duniani ".

"Ningefurahi Wayne Rooney ajiunge na Bayern,".

Pep Guardiola ambaye anajipanga kuelekea Allianz Arena kuanza kazi rasmi mwanzoni mwa msimu, angependelea kupewa bajeti ya uhamisho wa wachezaji ili kujenga kikosi imara.



Gerrard anasaka mafaniko ya kumaliza vema msimu kwa kupata nafasi nne za juu.

Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard amewataka wachezaji wenzake kukaza buti na kuhakikisha wanapata matokeo mazuri ili kumaliza katika moja ya nafasi nne za juu na kupata nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa Ulaya.

Wekundu hao wamefanikiwa kushinda michezo mitatu ikiwa ni pamoja na ushindi dhidi ya Tottenham Jumapili katika dimba la Anfield.

Gerrard anaamini ushindi utaipatia klabu hiyo imani na kuongeza kasi ya kusonga mbele kwenye changamoto ya ligi ya hiyo kusaka nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa Ulaya.

Kwasasa Liverpool iko katika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi, ikiwa ni alama saba nyuma ya Chelsea wanaoshika nafasi ya nne na ambao wanamichezo zaidi ya Liverpool.

No comments:

Post a Comment