KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, June 17, 2013

Liverpool kumalizana na Henrikh Mkhitaryan wa Shakhtar Donetsk



Liverpool inaendelea na jitihada zake za mpango wa kumsajili kiungo wa Armenian Henrikh Mkhitaryan katika moja ya usajili wao mkubwa kipindi hiki cha uhamisho wa kiangazi.
 Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 huenda akaihama klabu hiyo kwa pauni milioni £20 kutoka kwenye mkataba wake wa sasa na Shakhtar Donetsk ya Urusi.

Imeelezwa kuwa Liverpool imeonyesha nia ya kufikia kiwango hicho.
Kiungo huyo amekuwa mchezaji bora wa Armenia katika miaka ya 2009, 2011 na 2012 mfululizo.

Maafisa wa Anfield wako katika hadhari ya kukumbana na upinzani wa kumpata Mkhitaryan, ambaye ameifungia Shakhtar jumla ya mabao 25 msimu uliopita lakini pia Liverpool wanaaamini kushinda upinzani wowote na kumshawishi kiungo huyo kujiunga nao.

Meneja Brendan Rodgers anaona kuwa Mkhitaryan, ambaye pia amekuwa akiuhusishwa na kujiunga na Juventus pamoja na Borussia Dortmund, kuwa usajili muhimu katika mipango yao ya kuongeza makali ya kikosi msimu ujao.

Mkhitaryan aliaanza kucheza soka katika klabu ya Pyunik nchini kwao Armenia ambayo aliifungia jumla ya magoli 30 katika jumla ya michezo 70 aliyoichezea klabu hiyo.

Alielekea Ukraine na kujiunga na Metalurh Donetsk kiangazi 2009 na baada ya kuifungia jumla ya magoli 12 katika jumla ya michezo 37 aliyoicheza akajiunga na Shakhtar August 2010.

Mkhitaryan aliinza kuichezea timu yake ya taifa January 2007 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Panama ambapo aliifungia jumla ya magoli 11 katika jumla ya michezo 38.

Wakati huo huo Liverpool imesalia katika mazungumzo na Sunderland kwa lengo la kumsajili mlinda mlango Simon Mignolet.

Liverpool wameweka mezani pauni milioni £8 ilhali Sunderland ikisalia na masimamo wa kutaka pauni milioni £10 ambayo itamaliza zoezi hilo.

Rodgers tayari ameshamsajili mlinzi wa Manchester City Kolo Toure na wanaendelea na mpango wa kumsaliji mshambuliaji wa Celta Vigo Iago Aspas.

No comments:

Post a Comment