KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, July 4, 2013

TANZANIA NA ENGLAND ZASHUKA VIWANGO VYA UBORA VYA FIFA, HUKU BRAZIL IKIPANDA KWA KASI YA AJABU, Kone akodolewa macho na Newcastle.Mchezaji wa zamani wa Brazil ambaye ni mkurugenzi wa michezo wa PSG, Leonardo afungiwa msimu mzima.Pengo la Tevez Manchester City kuzibwa na Alvaro Negredo wa Sevilla.Ryan Giggs sasa kocha mchezaji wa United huku Phil Neville akipewa kazi ya ukocha wa kikosi cha kwanza. .......................Soma

Mshambuliaji Arouna Kone
Timu ya Newcastle inatafuta kwa udi na uvumba kuapata siani ya mshambuliaji wa Wigan Arouna Kone.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alishinda magoli 11 katika ligi kuu ya England na kushinda kombe la FA lakini anataka kuihama timu hiyo baada ya kushushwa daraja.
NewCastle ina upinzani wa Evarton ambayo nayo imekuwa ikitaka kumsajiri.Lakini Meneja wa Wigan Owen Coyle amesema mshambuliaji huyo kutoka IvoryCoast , yeye anagependelea kuhamia Everton.
"Ninaamini kupitia mwakilishi wake kuwa Everton ndiko anakotaka kuhamia"alisema Coyle.
Arouna Kone alisaini mkataba wa miaka mitatu alipojiunga na Wigan kutoka Levante ya Uhispania msimu uliopita na alikuwa kwenye kikosi kilichonyakua ushindi mkubwa wa kwanza kwa timu hiyo,waliposhinda Manchester City goli 1-0 katika fainali ya kombe la FA mwezi Mei mwaka huu.

Ryan Giggs sasa kocha mchezaji wa United huku Phil Neville akipewa kazi ya ukocha wa kikosi cha kwanza.
Manchester United imemtangaza Ryan Giggs kuwa kocha mchezaji huku Phil Neville akitarajiwa kutangazwa kuwa kocha wa kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Giggs ambaye anatarajiwa kufikia umri wa miaka 40 mwezi Novemba na mchezaji mwenzake wa zamani wa klabu hiyo Neville ambaye kwasasa ana umri wa miaka 36 ndio nyongeza mpya ya kocha mpya David Moyes katika safu ya watu wake wa pembeni katika benchi la ufundi Old Trafford.
Amekaririwa Moyes akisema
"Nimefurahi kwamba Ryan amekubali nafasi hiyo ya kuwa kocha mchezaji".
Kwa upande wake Giggs ameongeza kwa kusema
"Siyo siri nilikuwa nikichukua ujuzi wangu. Naliona hili kama ni hatua yangu ya mwanzo kwa hatma yangu ya baadaye katika soka"
Ilitazamiwa kuwa klabu hiyo ingemtangaza Nevile mwenye umri wa miaka 36 kuwa kocha mpya wa kikosi cha kwanza kufuatia kuondoka klabu hapo kwa Rene Meulensteen.
Giggs amendelea kwa kusema
"Ni fahari kubwa kuajiriwa kama kocha mchezaji. Nina matumaini nitaweza kuleta ujuzi wangu karibu, nikifanya kazi kama mchezaji na sehemu ya familia ya Manchester United kwa kipindi kirefu.
"Naangalia mbele kufanya kazi sambamba na David na timu"
Moyes ambaye alitajwa na mtangulizi wake Sir Alex Ferguson mwezi Mei, atafanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza hapo kesho Ijumaa kama meneja.
Kiungo Giggs alisaini mkataba mwingine wa kuongeza msimu mwingine wa mwaka mmoja kama mchezaji ndani ya United mwezi machi, mkataba ambao  utamuweka Old Trafford mpaka Juni 2014 ambapo atakuwa akikamilisha misimu 23 ya kuitumikia klabu hiyo.

 Pengo la Tevez Manchester City kuzibwa na Alvaro Negredo wa Sevilla.
 Manchester City imeonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji wa Sevilla ya Hispania Alvaro Negredo kuziba nafasi ya Carlos Tevez baada ya kutimkia Juventus.
Negredo mwenye umri wa miaka 27, amekadiriwa kwa thamani ya pauni milioni 24 huku City wakiwa na matumaini ya kumnasa kwa thamani pungufu ya hiyo.
Atletico Madrid walikuwa na mpanago wa kumchukua Negredo, lakini meneja mpya wa City Manuel Pellegrini ameweka wazi kuwa huyo ndiye mchezaji satahili kuziba pengo la Tevez.
Everton na West Ham hivi karibuni nao walikuwa wameonyesha nia lakini mshambuliaji huyo alidhihirisha kuwa ni wa thamni kubwa kwa vilabu vyote viwili.
Fernandinho na Jesus Navas tayari wameshawasili wakitoka katika vilabu vya Shakhtar Donetsk na Sevilla majira haya ya kingazi wakati City wakiimarisha kikosi chao kwa ajili ya kuchukua taji la ligi kuu ya England waliloliacha kwa Manchester United msimu uliopita.
Manchester City pia imekuwa ikihusihswa na mshambuliaji wa Benfica  Oscar Cardozo katika harakati zao za kuimarisha kikosi chao katika sehemu ya ushambuliaji baada ya kumuuza Mario Balotelli alielekea AC Milan ya Italia mwezi Januari.
Sergio Aguero amekubali mpango wa muda mrefu na Etihad, wakati ambapo inaaminika kuwa Pellegrini anataka kufanya kazi na Edin Dzeko ambaye hakuwa na wakati mzuri chini ya meneja aliyetangulia Roberto Mancini msimu uliopita.

 Mchezaji wa zamani wa Brazil ambaye ni mkurugenzi wa michezo wa PSG, Leonardo afungiwa msimu mzima.
 Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya Paris St-Germain ya Ufaransa Leonardo Nascimento de Araújo, maarufu kama Leonardo ambaye alikuwa kikaangani kwa kosa la kinidhamu kufuatia kumsukuma mwamuzi adhabu yake sasa imeongezeka na kufikia kusimama kwa miezi 13 ambayo ni wazi itamuweka pembeni kujishughulisha na soka kwa kipindi chote cha msimu ujao.
Kiungo huyo wa zamani wa Brazil mwenye umri wa miaka 43, hapo kabla alifungiwa kwa miezi tisa adhabu iliyotangazwa mwezi Mei.
Leonardo alionekana katika picha akitumia bega lake kugusana kwa lengo la kumsukumiza Alexandre Castro kufuatia kukasirishwa na kadi nyekundu aliyoonyeshwa Thiago Silva katika mchezo baina ya PSG na Valenciennes uliomalizika kwa sare ya bao 1-1.
Alikata rufaa lakini kwasasa amefungiwa kujishughulisha na shughuli zote za kiofisi mpaka juni 30 2014.
Leonardo ambaye aliwahi kusimamishwa kwa kusimama katika mstari wa unaogawa uwanja katika moja ya michezo ya PSG anatarajiwa sasa kurejea kazini mwezi February lakini kwasasa ataukosa msimu mzima.
Sambamba na adhabu hiyo, klabu hiyo ambao ni mabingwa wa Ufarasna wamekumbwa na adhabu ya kupokwa alama tatu katika kampeni ya ligi ya msimu ujao wa 2013-14.
Leonardo ambaye alikuwa kikosini wakati Brazil ikishinda taji la kombe la dunia mwaka 1994, amekanusha kumsukuma mwamuzi lakini hata hivyo alionekana na hatia ya kufanya hivyo huku ajitetea kwa kusema afisa mwingine aliyekuwa karibu yake kwa bahati mbaya alimsukuma kuelekea kwa mwamuzi Castro.
Mabingwa hao wa ligi ya Ufaransa PSG wamemwajiri Laurent Blanc kuwa bosi mpya mwezi uliopita baada ya Carlo Ancelotti kuelekea Real Madrid.

TANZANIA NA ENGLAND ZASHUKA VIWANGO VYA UBORA VYA FIFA, HUKU BRAZIL IKIPANDA KWA KASI YA AJABU

 England imeshuka katika viwango vya ubora vinavyo tambuliwa na fifa mpaka nafasi ya 15 kwa mujibu wa viwango vipya vya ubora ikiwa ni nafasi ya chini kutokea tangu waliposhindwa kufuzu kwa michuano ya Ulaya ya mwaka 2008
Kushuka huko kwa nafasi sita kuna maanisha kuwa kikosi cha meneja Roy Hodgson sasa kimepitwa na Bosnia-Herzegovina, Ivory Coast na Greece katika msimamo wa ubora wa viwango vya soka duniani.
Scotland imepanda kwa nafasi 24 mpaka kufikia nafasi ya 50 wakati ambapo Ireland ya Kaskazini imepanda kwa nafasi tano kutoka katika nafasi ya 111 ya mwezi Juni
Wales imeshuka kwa nafasi moja mpaka nafasi ya 46 na Jamhuri ya Ireland ikishuka kwa nafasi tatu mpaka nafasi ya 44.

Wakati hayo yakiwa hivyo soka la tanzania limeshuka kwa nafasi tatu baada ya kupungukiwa alama 12 na sasa inashika nafasi ya 35 kwa mwezi huu wa Machi tofauti na ilivyokuwa mwezi wa juni ambapo ilikuwa imeshika nafasi ya 32.

Tanzania imepoteza alama nyingi za mwezi uliopita kufuatia kufungwa katika michezo miwili muhimu ya kusaka nafasi ya kufuzu kwa fainali ya kombe la dunia.

Stars ilifungwa na Morocco kwa mabao 3-1 katika mchezo uliofanyika nchini Morocco kabla ya kufungwa na Ivory Coast katika mchezo mwingine uliofanyika Tanzania.

Katika hali iliyotazamiwa na wengi ni kwamba Brazil imepanda kwa kasi kubwa kutoka nafasi ya 15 iliyokuwepo mwezi uliopita mpaka kufikia nafasi ya 9 mwezi huu.

Matokeo mazuri ya kupanda kwa Brazil yametokana na mafanikio iliyo yapata katika michezo ya kuwania kombe la shirikisho pamoja na michezo yake ya hivi karibuni ya kimashindano na kirafiki.
 
Kwa upande wa soka la wanawake, England imepanda kwa nafasi moja ikishika nafasi ya saba huku Scotland wakipanda mpaka nafasi ya 21. Wales kwasasa wako katika nafasi ya 37 huku Ireland ya kaskazini ikishika nafasi 54.

Bofya msimamo kamili kulia fifa Ranking.

No comments:

Post a Comment