KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 29, 2013

TIAGO SILVA AWAMALIZA KABISA BARCELONA YENYE MATATIZO SEHEMU YA ULINZI WA KATI.


Mlinzi wa kati aliyekuwa anawindwa na Barcelona Thiago Silva amesaini mkataba mwingine wa nyongeza na klabu yake ya nchini Ufaransa ya Paris St-Germain.

Mlinzi huyo wa kati alijiunga na mabingwa hao wa ligi ya Ufaransa mwaka 2012 kwa ada ya uhamisho ya pauni  £36m, kwa mkataba wa miaka mitano na sasa akitarajiwa kumaliza mkataba huo mwaka 2018.

Barcelona ilikuwa ikitarajiwa kumsajili  nyota huyo wa kimataifa mwenye umri wa miaka 28 raia wa Brazil lakini suala la maslahi limeendelea kumbakisha ndani ya klabu yake ya PSG.

Mlinzi mkongwe wa Barca Carles Puyol mwenye umri wa miaka 35 amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya mguu tangu mwezi March, wakati ambapo mlinzi Gerard Pique, Adriano Correia na Javier Mascherano wamekuwa mareruhi.

Barcelona imekuwa ikihusishwa na mlinzi mwingine wa kimataifa wa Brazil kutoka klabu ya Chelsea David Luiz, lakini mwezi Juni wakakanusha kuwa hawakuwa katika mawindo ya kumsajili mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 26 wakati huo Tito Vilanova akiwa katika benchi la ufundi.

No comments:

Post a Comment