KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, October 7, 2013

BABU FRANCESCO TOTTI AMSUUZA MARCO MATERAZZI NA KUDHANI KUWA ATACHEZA SOKA MPAKA MIAKA 45.

Nyota wa klabu ya Roma Francesco Totti anaweza kucheza soka mpaka atakapo fikia umri wa miaka 45 hii ni kauli ambayo imetolewa na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Italia Marco Materazzi.

Mshambuliaji Totti ambaye kwasasa yuko katika umri wa miaka 37 yuko katika kiwango cha kusisimua na cha kuvutia baada ya kufunga magoli mawili katika mchezo wa jumamosi ambao Roma walichomoza na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Inter na kuamsha kuitwa tena katika kikosi cha timu ya taifa ya Italia maarufu kama Azzurri , ikiwa ni baada ya miaka saba kupita baada ya kushinda taji la dunia nchini Ujerumani mwaka 2006.

Materazzi alivutiwa sana na Totti na wala hakushangazwa na kiwango cha juu cha Totti katika dimba la San Siro na kudhani kuwa mkongwe huyo wa Giallorossi kuwa ana kipaji na mbinu za kuendelea kucheza soka katika kiwango cha juu kwa muda mrefu licha ya umri wake kuendelea kukata kona.

Amenukuliwa Matereza akiongea na Tele Radio Stereo akisema
"Totti can play until he's 45,".

"Si rahisi wakati umri unayoyoma ingawa una kuwa unapunguza kasi lakini muhimu ni akili.

"Alichokifanya hakikunishangaza mimi, pengine ianweza ikawa shangaza watu wengine kutokana na umri wake.

"Lakini -What he does on the pitch is so natural-."

Totti atakuwa kivutio katika mchezo wa ligi kuu ya Italia Serie A kuelekea katika mchezo wa Oktoba 19 dhidi ya Napoli.

No comments:

Post a Comment