KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, October 8, 2013

Gus Poyet bossi mpya wa Sunderland

Klabu ya Sunderland ya Egland imemteua Kocha wa zamani wa Brighton, Gus Poyet kuwa kocha mpya wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu hiyo ambayo inajulikana kama "The Black Cats " inashikilia mkia katika ligi kuu ya Premier na ilimuondosha kazini Paolo Di Canio mnamo mwezi wa September baada ya kushikilia nafasi hiyo kwa mechi 13 tu.
"nina hamu ya kuwathibitishia uwezo wangu mashabiki--ninataka wawe na imani kwa sababu tunahitaji kushikamana " Poyet, mwenye umri wa miaka 45, ameiambia wavuti wa klabu hiyo.
Ataungana na wasaidizi wake za zamani wa Brighton, Mauricio Taricco na Charlie Oatway.
"Nadhani msingi wa mafanikio yangu katika mechi za nyumbani Brighton ni uhusiano wangu na mashabiki, --na naweza kuona hali hiyo hiyo hapa ,"aliongeza Poyet, ambaye alipigwa kalamu na Brighton mnamo mwezi wa Juni.
"ni changamoto kubwa lakini inanipa motisha na nashukuru kwa kupata fursa hii ya kuongoza katika ligi kuu"
Poyet ambaye ni mchezaji wa zamani wa taifa wa timu ya Uruguay atakua meneja wa sita wa Sunderland katika kipindi cha miaka mitano.
Kocha msaidizi wa Sunderland Kevin Ball amekua akishikilia uongozi wa klabu hiyo tangu Di Canio afutwe kazi kutokana na malalamiko ya wachezaji.

No comments:

Post a Comment