KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, October 31, 2013

VITI VYANG'OLEWA UWANJA WA TAIFA BAADA YA BAO LA KUSAWAZISHA LA KAGERA DHIDI YA SIMBA.

Polisi jijini Dar es Salaam Tanzania wamelazimika kutumia Mabomu ya machozi kuwatawanya mashabiki wa Klabu ya Simba, baada ya kumalizika mechi ya Ligi kuu soka Tanzania bara hii leo kwa matokeo ya sare baina ya Simba na Kagera Sugar.
Vurugu hizo zimezuka mwishoni mwa mechi ambayo timu ya Simba imezidi kuporomoka hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo kufuatia matokeo ya sare ya bao 1-1.

Baada ya Simba kuongoza bao 1 hadi dakika ya 90 Kagera Sugar walisawazisha kwa Penati iliyotiwa kimiani na beki wa zamani wa Simba Salum Kanoni ambapo mashabiki wanaoaminika kuwa wa Simba walianza kung'oa viti uwanjani hali iliyosababisha askari polisi kurusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya mashabiki hao.

Simba ilianza kuliona lango la Kagera Sugar katika dakika ya 45 baada ya mshambuliaji raia wa Burundi Amis Tambwe kufunga bao la kwanza lililodumu hadi mapumziko.

Katika Kipindi cha pili Simba walianza kucheza kwa kujihami hali iliyosababishga Kagera kukaribia lango lao mara kwa mara na hatimaye wakafanikiwa kusawazisha katika dakika ya 90.

Kwa matokeo hayo Simba imeporomoka hadi nafasi ya nne wakiwa na pointi 21,huku Azam, wakishika nafasi ya kwanza kwa kuwa na pointi 23 sawa na Mbeya City lakini wakitofautiana kwa magoli ya kufunga.
Yanga ni ya tatu kwa kuwa na pointi 22.

No comments:

Post a Comment