Bayern Munich imevunja rekodi ya Hamburg SV ya kipindi kirefu ya kucheza michezo 36
ya ligi kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga bila kufungwa baada ya hapo jana kuichapa Augsburg mabao 3-0.
Itakumbukwa The Bavarians walitwaa taji la Ujerumani msimu uliopita wakipoteza mchezo mmoja ugenini na pia kufungwa nyumbani na Bayer Leverkusen 2-1 Novemba mwaka jana.
Walimaliza kwa ujumla wa alama 25 mbele ya wanaowafuatao Borussia Dortmund na sasa wameanza kupaa tena katika msimu huu wakishinda michezo yote isipokuwa michezo miwili ambayo wamekwenda sare dhidi ya B04 na Freiburg.
Itakumbukwa The Bavarians walitwaa taji la Ujerumani msimu uliopita wakipoteza mchezo mmoja ugenini na pia kufungwa nyumbani na Bayer Leverkusen 2-1 Novemba mwaka jana.
Walimaliza kwa ujumla wa alama 25 mbele ya wanaowafuatao Borussia Dortmund na sasa wameanza kupaa tena katika msimu huu wakishinda michezo yote isipokuwa michezo miwili ambayo wamekwenda sare dhidi ya B04 na Freiburg.
No comments:
Post a Comment