Akiwa mchezaji wa zamani wa timu ya vijana ya AC MILAN, soka la
Pierre Emerick Aubameyang lilianza kuchomoza baada ya kujiunga na klabu
ya Saint Etienne kwa mkataba wa kudumu mnamo mwaka 2011.
Lakini mkataba huo ulimalizika Julai
baada ya kujiunga na washindi wa pili wa Kombe la Klabu Bingwa Barani
Ulaya, Borussia Dortmund , akichukua nafasi ya Mario Gotze, baada ya
uhamisho wake uliotarajiwa sana kwenda Bayern Munich.
Lakini mkataba wake na Les Verts ulimalizika kwa
mtindo wa aina yake, kwani kalbu hiyo ilishinda taji la French League
One kwa mwaka 2013, hivyo kumwezesha Aubameyang , kupata tuzo yake ya
kwanza kama mchezaji wa kulipwa.
Ingawa hakufunga goli katika mchezo huo, lakini
aliwahi kuzifumania nyavy mara 19, katika ligi kuu ya Ufaransa , huku
mchezaji wa PSG, Zlatan Ibrahmovic, akiongoza kwa mabao, na mchezaji
huyo kutoka Gabon akiwa ametoa pasi nane zilizozaa mabao.
Uchezaji huo mahiri ndio ulioishawishi Dortmund, kumnunua kwa kitita cha Paundi milioni 11 kwa mkataba wa miaka mitano.
Na mara alijiongezea tuzo, baada ya Dortmund
kulipiza kisasi cha kufungwa katika fainali ya Klabu Bingwa Barani Ulaya
jijini London mnamo Mei, kwa kuwafunga mahasimu wao Bayern Munich mabao
4 -2 hivyo kutwaa taji la Supercup la ufunguzi wa msimu wa Ligi Kuu ya
Ujerumani.
Aliibuka na kuwa mchezaji wa sita kufunga mabao
matatu peke yake yaani ‘Hat Trick’ katika mchezo wake wa kwanza akiwa na
Dortmund ilipocheza na Ausburg na kuifunga mabao 4 – 0.
Magoli yaliendelea kutiririka huku Aubameyang
akijipanga vilivyo hasa kutokana na kuzifumania nyavu mara saba katika
mechi 11 alizocheza katika klabu inayofundishwa na Jurgen Klopp.
Wakati soka lake kwa upande wa klabu liliendelea
kukua kwa mwanasoka huyo mwenye umri wa miaka 24, mwaka 2013 ulikuwa si
wa kuridhisha upande wa kimataifa.
Hata hivyo, mwanga ulichomoza tena pale
alipopachika ‘Hat Trick’ kwa njia ya penalty dhidi ya Niger katika
mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia mnamo mwezi Juni, lakini huo ulikuwa
ushindi pekee wa timu ya taifa ya Gabon maarufu kama ‘Panthers’ na
kushika nafasi ya tatu katika kundi lao, hivyo kufuta matumaini ya
kushiriki Kombe la Dunia litakalofanyika nchini Brazil mnako 2014.
Maoni ya wadadisi wa soka kumhusu Emerick
Mshambuliaji huyo wa Gabon alifunga ‘Hat Trick’
dhidi ya klabu ya Augsburg katika mechi ya ufunguzi ya msimu mpya na
kudhiirisha moja kwa moja kwa mashabiki kwamba, alistahili kununuliwa
kwa Paundi milioni 11 na kujiunga na klabu hiyo ya Ujerumani.
Huo kimsingi utakuwa ulikuwa mwaka muhimu kwa mshambulijai huyo mwenye miaka 24
Mnamo mwaka 2012, alivutia katika michuano ya
Kombe la Mataifa ya Afrika, iliyofanyika nchini mwake na baada ye
alighairi kujiunga na Tottenham Hotspur.
Hivyo 2013, Aubemeyang alilazimika kudhiirisha kwamba, anaweza kufikia kiwango cha juu , na kweli alifanya hivyo .
Bao lake la St Etienne, katika ushindi wa timu
yake wa mabao 3 – 0 dhidi ya Bastia mnamo Januari, ulikuwa ni mwanzo wa
mfululizo wa kupachika mabao ambao ulimfanya azifumanie nyavu katika
mechi saba za Ligi Kuu ya Ufaransa.
Aubameyang alimaliza msimu akiwa amepachika
mabao 19 katika ligi, na pia alitoa pasi iliyozaa bao la ushindi katika
fainali ya Kombe la Ligi la Ufaransa, baada ya St – Etienne kushinda
kombe muhimu baada ya miaka thelathini.
Alihusishwa na kujiunga na klabu kubwa katika
majira ya joto na mengi yanasemwa kuhusu kiwango chake cha usakataji
kabumbu, na kwamba, Borussia Dortmund, timu ambayo iliifunga Real Madrid
ili kufikia fainali ya Kombe la Klabu Bingwa Ulaya, ilipambana vilivyo
kupata saini ya mwanandinga huyo.
Inawezekana Aubameyang hapangwi katika kikosi
kinachoanza pale timu yake inapocheza kwa sasa, lakini Jurgen Klopp,
mpishi wa mafanikio ya Dortmund, anasema tayari ameonesha mafanikio
makubwa na kuvutia, katika moja ya vilabu vyenye kipaji Barani Ulaya.
Moja ya mafanikio hayo ni pamoja na kufanikiwa
kukimbia muda wa haraka zaidi kwa mita thelathini kuliko bingwa wa mbio
za mita 100 duniani Usain Bolt.
Licha ya juhudi kubwa za Aubameyang, timu ya
taifa ya Gabon imeshindwa kuonesha cheche kwa mwaka 2013, lakini kwa
upande wa klabu umekuwa ni mwaka wa mafanikio kwa mshambuliaji huyo.
Na hivyo basi nitampigia kura kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika wa BBC kwa mwaka 2013.
No comments:
Post a Comment