Majina ya wanaowania taji la BBC la mchezaji bora zaidi barani Afrika
mwaka wa 2013 yametangazwa rasmi hii leo kupitia kipindi cha kiswahili
cha Amka na BBC
Yaya Toure wa Ivory Coast yuko katika orodha hiyo kwa mara ya tano mtawalia, wengine katika orodha hiyo ni Victor Moses na John Mikel Obi wa Nigeria, Jonathan Pitripia wa Bukina Faso na Pierre- Emerick Aubameyang wa Gabon.
Mshindi atateuliwa na mashabiki wa kandanda ambapo watapiga kura hadi tarehe 25 Novemba saa tatu usiku saa za Afrika Mashariki
Unaweza kupiga kura kwenye tovuti hii ama kwa kutuma ujumbe mfupi kupitia nambari ifuatayo +44 7786 20 20 08:
Tuma 1 ili kumpigia kura Pierre-Emerick Aubameyang
Tuma 2 ili kumpigia kura Victor Moses
Tuma 3 ili kumpigia kura John Mikel Obi
Tuma 4 ili kumpigia kura Jonathan Pitroipa
Tuma 5 ili kumpigia kura Yaya Toure
Gharama ya ujumbe ni kulingana na kanuni za
kimataifa tafadhali thibitisha na mhudumu wako.
Ni sharti utume ujumbe
mmoja pekee kwa kila nambari ya simu.
Mshindi atatangazwa Jumatatu tarehe 2
Disemba saa Mbili na dakika thelathini na tano Usiku saa za Afrika
Mashariki katika kipindi cha BBC cha (Focus on Africa) katika redio na
runinga.
Hakuna mchezaji katika orodha ya mwaka huu
aliyeteuliwa kutokana na kura za wanahabari 44 wa Afrika amewahi
kushinda shindano hili la BBC.
Wawili kati yao – Jonathan Pitroipa na
Pierre- Emerick Aubameyang- ndio wa kwanza katika orodha hiyo kutoka
mataifa yao.
Aubameyang, mwenye miaka
24,amekuwa mchezaji mzuri sana katika kipindi cha mwaka mmoja
uliopita-na kumaliza msimu wa mwaka 2012-2013 akiwa ameingizia klabu
yake St-Etienne mabao 19, na kumweka wa pli, kwenye orodha ya wachezaji
bora zaidi kwenye ligi ya Ufaransa. Alisaidia klabu yake kushinda kombe
lake la kwanza.
Walioteuliwa kuwania taji la BBC la mchezaji bora Afrika
Pierre-Emerick Aubameyang
Victor Moses profile
John Mikel Obi
Jonathan Pitroipa
Yaya Toure
Victor Moses profile
John Mikel Obi
Jonathan Pitroipa
Yaya Toure
Mchezo wake ulimuwezesha kuhamia klabu ya Borussia Dortmund, na tayari ameingizia klabu hiyo ya Ujerumani mabao 11.
Mchezo wa Pitroipa ulianza
kushika kasi alip[otajwa kuwa mcherzaji bora wakati wa michuano ya taifa
bingwa Afrika iliyochezwa nchini Afrika Kusini ambapo pia alisaidia
Burkina Faso kufika fainali ya michuano hiyo.
Pitroipa ameendelea kunga'aa na hata kuingizia
nchi yake mabao matatu katika michuano ya kuwania nafasi ya kushiriki
kwenye kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil.
Wachezaji wawili walifanya hata vyema zaidi
katika kombe la mataifa bingwa mwaka huu; ni pamoja na Mikel na Moses
wote waliohusika pakubwa katika kufanikisha mchezo wa Nigeria hadi
wakashinda kombe hilo mara ya kwanza katika miaka 19.
John Mikel Obi, mwenye umri wa
miaka 26, pia alishinda kombe la Uropa akichezea Chelsea, wakati mwaka
2013 ndipo aliweza kuingizia Chelsea bao lake la kwanza baada ya kucheza
mechi 185.
Mabao yamekuwa yakija kwa kasi kwa mchezaji VictorMoses
mwenye umri wa miaka 22 huku akiingizia Chelsea mabao sita kabla ya
kuhamia Liverpool, alikoingiza bao lake la kwanza mwezi Septemba.
Yote tisa, kumi ni kuwa mchezaji mwingine nyota ni Yaya Toure ambaye ni kiungo cha kati. Toure mwenye umri wa miaka 30, raia wa Ivory Coast, ameingiza mabao 12 hadi sasa mwaka huu pekee.
Ingawa yeye na wachezaji wenzake wa Man City,
walipokonywa ushindi wa ligi ya Premier msimu uliopita, Toure bado
alikuwa ngome imara uwanjani , huku akiwika sana mbele ya lango la bao.
No comments:
Post a Comment