KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, January 13, 2014

AC Milan yamtimua kocha Allegri

Klabu ya Ac Milan imemfuta kazi Massimiliano Allegri na kumpandisha ngazi Mauro Tassotti kama kocha wa muda, baada ya vigogo hao wa soka Italia kuwa na mfululizo wa matokeo mabaya katika Serie A 
Uamuzi huo umekuja siku moja baada ya vigogo hao wa soka kuabishwa kwa kupewa kichapo cha mabao 4-3 na klabu iliyopandishwa ngazi msimu huu Sassulo.
Huku wakiwa katika nafasi ya kumi na moja kwenye msimamo wa ligi kuu ya Italia Serie A, Milan wametangaza uamuzi huo kupitia tovuti yao. 
 Wameshinda mechi 19 pekee msimu huu na Allegry alikuwa tayari ametangaza katika kipindi kifupi cha mapumziko ya majira ya baridi kuwa huenda akaondoka mwishoni mwa msimu.
AC Milan ndio wawakilishi pekee wa Italia katika Champions League katika awamu ya mchujo AC Milan ndio wawakilishi pekee wa Italia katika Champions League katika awamu ya mchujo

Allegri alichukua usukani mnamo mwaka wa 2010 na akashinda Serie A katika msimu wake wa kwanza kisha akamaliza katika nafasi za pili na tatu katika misimu iliyofuata. Hata hivyo, AC Milan ndio timu pekee ya Italia kufuzu kazika awamu ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, na watapambana na Atletico Madrid mwezi ujao.
Kwingineko, barani Ulaya, Real Madrid waliitumia faida ya mchuano uliotoka sare kati ya viongozi wa La liga Atletico Madrid na Barcelona kwa kusajili ushindi wa goli moja kwa sifuri nyumbani kwa Espanyol na kupunguza pengo baina ya viongozi hao hadi pointi tatu pekee..wakati ikiwa imefikia nusu ya msimu. Bao la kichwa alililofunga Pepe lilitosha kuwapa Madrid pointi tatu na sasa wako katika nafasi ya tatu na pointi 47.
Kule England, Manchester City walisonga hali kileleni mwa Premier League, baada ya kupata ushindi wa magoli mawili kwa sifuri dhidi ya Newcastle baada ya Chelsea kushikilia usukani kwa siku moja kufuatia ushindi wao wa magoli mawili kwa sifuri dhidi ya Hull.
Arsenal waliteremka hadi nafasi ya tatu lakini leo wanaweza tena kurejea kileleni, kama watawashinda Aston Villa. Kwingineko magoli yalizidi kutiririka kwa upande wa Liverpool ambao wako katika nafasi ya nne, baada ya Luis Suarez kufunga mawili katika ushindi wao wa magoli matano kwa matatu dhidi ya Stoke.

No comments:

Post a Comment