KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, January 6, 2014

Dunia bado inaendelea kuomboleza kifo cha 'Chui Mweusi' Eusebio da Silva Ferreira

Buriani Chui mweusi , Eusebio da Silva Ferreira, wapenzi wa soka duniani kote wamlilia mchezaji huyo nyota mzaliwa wa Msumbiji aliyefariki jana Jumapili(05.01.2014) nchini Ureno. 

 Eusebio da Silva Perreira , maarufu kama Eusebio ama jina la utani "Chui mweusi", amefariki jana Jumapili akiwa na umri wa miaka 71, na kifo chake kimewaletea mashabiki wengi simanzi , wakimkumbuka nyota huyo ambaye alitokea katika bara la Afrika nchini Msumbiji na kuwa mmoja kati ya wachezaji nyota duniani.
Eusebio aliyefariki siku ya Jumapili asubuhi kutokana na moyo wake kushindwa kufanyakazi, alitawala soka nchini Ureno katika miaka ya 1960, na kuiletea sifa nchi hiyo pamoja na klabu yake ya Benfica Lisbon. Serikali ya Ureno imetangaza siku tatu za maombolezo, na bendera mjini Lisbon zinapepea nusu mlingoti kabla ya mazishi yake siku ya Jumatatu ambapo mamia kwa maelfu ya watu wanatarajiwa kujipanga mitaani kutoa heshima zao za mwisho.
Portugals Fußball-Legende Eusebio ist tot Eusebio akiwa na Ronaldo (kulia)

Wachezaji kadha wa zamani ikiwa ni pamoja na Bobby Chalton ambaye aliisaidia Manchester United kupata ushindi dhidi ya Benfica katika mwaka 1968 katika fainali ya kombe la Ulaya ambalo sasa ni champions League , amesema ilikuwa ni nafasi ya pekee kumfahamu Eusebio. Franz Beckenbeuer nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani katika kombe la dunia 1970 , 74 na 78 amemueleza Eusebio kama rafiki yake na nyota wa wakati huo.
Kwa wengi Eusebio aliyezaliwa mwaka 1942 nchini Msumbiji hadi leo hii ndie mchezaji bora kabisa katika historia ya soka nchini Ureno na mchezaji wa kwanza nyota kutoka bara la Afrika. Ameisaidia timu yake ya Benfica kupata mafanikio kadha kitaifa na kimataifa. Mwandishi wa habari za michezo mzaliwa wa Msumbiji Jose Musuaili alimpenda sana Eusebio tangu akiwa mtoto , licha ya kuwa yeye binafsi alikuwa shabiki mkubwa wa timu hasimu nchini Ureno ya Sporting Lisbon.
Bildergalerie Fußballer Eusebio Eusebio da Silva Ferreira

"Alikuwa kipenzi cha kizazi chote cha baba zetu. Na hata leo ni alama maalum kwetu. Sio tu kwa wapenzi wa soka kwa sisi Waafrika, lakini pia kwa watu wote, ambao wanazungumza lugha ya Kireno. Nimebahatika, kuwa rafiki wa familia ya Eusebio. Katika mahojiano yangu ya kwanza na Eusebio , nilitambua kuwa Eusebio kwa kweli yuko kama tunavyomuona. Kwa upande mmoja ni nyota wa soka la Ureno na kimataifa, lakini kwa upande mwingine ni mtu wa kawaida kabisa."
Bildergalerie Fußballer Eusebio Eusebio akifunga bao

Eusebio aliichezea Ureno mara 64 alifunga mabao 41. Pia alituzwa kiatu cha dhahabu mara mbili na amekuwa mfungaji bora nchini Ureno kati ya mwaka 1964 na 1973. Aliipatia ushindi wa ligi Benfica mara 11 pamoja na vikombe vitano vya chama cha mpira nchini Ureno. Aliistaafu soka mwaka 1979. Mungu amlaze mahali pema . Ameen.

No comments:

Post a Comment