KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, January 6, 2014

Habari na matukio mengi ya michezo ya soka. Bofya kusoma zaidi

Frank Ribery( kulia)
Vilabu vinavyoshiriki ligi ya Ujerumani Bundesliga ambayo iko mapumzikoni hivi sasa vimeanza rasmi kambi ya mazoezi wiki hii. 
 Mabingwa wa Bundesliga Bayern Munich na Schalke 04 wako nchini Dubai , makamu bingwa Borussia Dortmund wanaanza kambi nchini Uhispania wiki ijayo na Bayer Leverkusen halikadhalika wako nchini Uhispania.

Lakini wakati taarifa hizo zikiarifu vivyo, ni kwamba mshambuliaji wa pembeni wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ufaransa Frank Ribery wakati huo huo ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa nusu ya kwanza ya ligi ya Ujerumani Bundesliga uteuzi uliofanywa na wachezaji wenzake wa ligi hiyo.

 Arjen Robben pia wa Bayern ameshika nafasi ya pili wakati Marco Reus wa Borussia Dortmund ameshika nafasi ya tatu.

Ligi nyingine Ulaya
Ligi za mataifa mengine hata hivyo zinaendelea , ambapo hapo jana Juventus Turin ilitunisha misuli yake dhidi ya Roma na kuirarua kwa mabao 3-0. Kabla ya hapo Fiorentina iliibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Livorno.

Matukio mengine
1)Matumaini ya mshambuliaji wa Italia Giuseppe Rossi kucheza katika kombe la dunia huenda yakatatizwa baada ya mchezaji huyo wa Fiorentina kupata maumivu katika goti lake la mguu wa kulia ambalo limekuwa na matatizo kila mara katika mchezo wa jana Jumapili dhidi ya Livorno.

2)Gareth Bale amepona maumivu katika mguu wake wa kushoto na atakuwamo katika kikosi cha Real Madrid ambacho kitashuka dimbani leo jioni kupambana na Celta Vigo.

3)Katika michezo ya jana Jumapili katika ligi ya Uhispania la Liga Barcelona iliirarua Elche kwa kuipa kipigo cha mabao 4-0. Ushindi huo wa Barca hata hivyo umekuja bila ya mshambuliaji wake hatari Lionel Messi.
Kocha wa Barcelona Gerardo Tata Martino amesisitiza hata hivyo kuwa hatamharakisha Messi kurejea uwanjani katika pambano la wababe walioko kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo dhidi ya Atletico Madrid mwishoni mwa juma lijalo. Messi hajacheza tangu alipoumia misuli katika mchezo dhidi ya Real Betis mapema mwezi Nivemba na alikuwa mtazamaji tu wakati mabingwa hao waliporejea kileleni mwa msimamo wa ligi jana katika ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Elche.

4)Manchester United itaangalia majaliwa yake katika kombe la ligi ili kurejesha imani kwa mashabiki katika msimu huu wakati watakapokuwa wageni wa Sunderland kesho Jumanne katika mchezo wa kwanza katika nusu fainali.

Jana Jumapili Manchester United iliangukia pua pale ilipoyaaga mashindano ya mwaka huu ya kombe la FA baada ya kuzabwa mabao 2-1 dhidi ya Swansea City katika uwanja wa nyumbani wa Theather of Dreams , Old Trafford.
Licha ya kuwa United bado inaendelea kucheza katika harusi mbili , ligi ya mabingwa wa Ulaya Champions League na kombe la ligi, kombe hilo ndio matumaini yao makubwa kuweza kuokoa msimu ambao unaonekana kuwa wa maafa.
FC Everton Trainer David Moyes David Moyes kocha wa Manchester United
Wakati kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson hatimaye alipobwaga manyanga katika kazi ya kuifunza timu hiyo alisimama katika nyasi za Old Trafford na kuwatafadhalisha mashabiki wa Man United kumpa ushirikiano na kumuunga mkono mrithi wake aliyemteua David Moyes kwa kukumbuka nyakati mbaya pamoja na zile nzuri.
Lakini baada ya jana Manchester United kunyofolewa kutoka katika kinyang'anyiro hicho cha kombe la FA mashabiki hawakusita kuonesha kufadhaika kwao.
Chelsea wamepangwa dhidi ya Stoke City katika kombe hilo la FA katika duru ya nne katika upangaji wa mchezo hiyo jana Jumapili. Liverpool ambayo iliiangusha Oldham Athletic kwa mabao 2-0 jana itawatembelea Bournermouth ama Burton Albion. Zawadi ya Swasea City kwa kuwaondoa Manchester United katika kinyang'anyiro hicho itakuwa ziara kwa Birmingham City , Bristol Rovers ama Crawley Town.

No comments:

Post a Comment