KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, January 9, 2014

Van Persie zimebaki siku kumi tu kurejea United rasmi

Robie van Persie anatarajiwa kurejea Manchester United ndani ya siku kumi baada ya kukamilisha wiki mbili za marekebisho ya ubora wa afya yake kimchezo alizopewa na mtaalamu wa viungo wa United akiwa nyumbani kwao Uholanzi.

Mshambuliaji huyo amekuwa akifanyakazi sambamba na kocha viungo wa PSV Eindhoven 'fitness coach' Arno Philips baada ya ya kuwa nje kwa muda sasa kutokana na kusumbuliwa na msuli tangu mapema mwezi Disemba.

Van Persie amekamilisha hatua ya mwisho ya ukarabati huo wa afya na sasa anarejea Manchester kuanza upya mazoezi katika viunga vya mazoezi vya klabu yake vya Carrington.

Taarifa zinaarifu kuwa Programu yake imeshakamilika kwa lengo la kumjenga upya taratibu kiafya ya mazoezi kabla ya kujiunga tena na kikosi cha kwanza.

No comments:

Post a Comment