KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, February 17, 2014

Swansea yaendelea kugomea ofa za vilabu kadhaa juu ya mlinzi Ben Davies licha ya mwenyewe kuonekana kuwa tayari kuondoka

Mlinzi wa kushoto wa Swansea Ben Davies (pichani kushoto) yuko katika mawindo ya vilabu vingi Ulaya
Mlinzi wa Swansea Ben Davies ameelezea kutakiwa na vilabu kadhaa vikubwa barani Ulaya licha ya kusaini mkataba mkataba wa miaka minne na nusu kabla ya Christmas.

Mlinzi huyo wa kimataifa wa Wales mwenye umri miaka 20 alikuwa akiwindwa na Manchester City, Liverpool, Arsenal na kwa mshangao mkubwa pia Atletico Madrid ilikuwa ikimuwinda katika siku za hivi karibuni.
 
Vilabu vyote hivyo vimeingia sokoni hivi sasa kusaka mlinzi wa kushoto

Davies amecheza zaidi ya michezo 60 tangu ajiunge na Swansea na akicheza mchezo wa kwanza katika mchezo dhidi ya West Ham mwezi Agosti 2012 ambapo uwezo wake umekuwa ukiongezeka kwa kasi.
Swansea imekuwa haitaki kumuuza mlinzi huyo na imekuwa ikionyesha uwezo wa kupingana na ofa kadhaa ikiwemo ya Fulham ambayo ilikuwa mpango mezani wa pauni milioni  £4 wakimtaka mchezaji mwenzake na Davies huyu si mwingine bali ni Neil Taylor mwezi uliopita.
No fall guy: Davies (right) has impressed despite Swansea's Premier League struggles this season
Davies (kulia) amekuwa akivutia licha ya uwezo mdogo wa klabu yake katika Premier League msimu huu

No comments:

Post a Comment