Kocha wa Cameroon Volker Finke amesema kurejea kwa kiwango cha uchezaji cha Samuel Eto'o ni nguvu kubwa kwa taifa hilo katika kampeni ya kombe la dunia.
Eto'o alisajiliwa Chlesea akitokea Anzi Makhachkala mwezi Agosti ambapo tangu wakati huo amekuwa akiimarika kiwango kiasi Finke kuvutiwa na anadhani kuwa uhamisho wa mshambuliaji huyo kuelekea katika ligi ya England umemsaidia sana mchezaji huyo mapoja na Cameroon pia.
"Nianfurahi ameachana na soka la Ki-Russia na sasa nadhani akiwa Chelsea amerejea katika kiwango bora" Amesema Finke.
"Nim mchezaji bora wa Cameroon na anaweza kuleta utoufi katika kombe la dunia."
Eto'o amefunga magoli nane katika michezo 26 aliyoichezea Blues, ikiwa ni pamoja na mchezo dhidi ya United ambapo alipiga hat-trick mwezi januari, lakini tangu wakati huo hajafunga tena goli katika michezo sita iliyopita.
No comments:
Post a Comment