KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, March 13, 2014

Kuelekea Soweto derby Jumamosi nchini Afrika kusini, mwamuzi mkongwe Ncobo anasema 'Nothing like the Soweto Derby' na habari nyingine kibao soma......

Mwamuzi wa zamani wa ligi kuu ya soka nchini Afrika kusini Andile ‘Ace’ Ncobo amezungumzia juu ya presha inayowakumba waamuzi wa mchezo mkubwa utakao pigwa Jumamosi mjini Soweto maarufu kama Soweto Derby baina ya Orlando Pirates dhidi ya Keizer Chiefs.
Ncobo ambaye pia ni meneja wa zamani wa PSL amesema katika soka nchini Afrika kusini hakuna kama Soweto Derby na kwamba jambo pekee ambalo litawasaidia waamuzi hao katika mchezo huo mkubwa nchini Afrika kusini ni kuwa vizuri kiakili(mentally tough).
“Uzoefu ni kitu bora, ni mchezo mkubwa katika kalenda ya soka la nchi hiyo bila kujali ni mchezo wa ligi, wa michuano tu, wa kirafiki, mchezo wa nje ya msimu yaani bado ni mchezo mkubwa”Ncobo alikuwa akiongea na SuperSport katika mahojiano.
“Najua makamishina wa mchezo na waamuzu watawaambia waamuzi hao kuuchukulia kama michezo mingine, lakini ukweli ni kwamba si kama michezo mingine.
“Unakuja na presha kubwa, na ni presha hiyo ndiyo inayoingia ndani, hutarajii nini kitatokea katika mchezo, huwezi kwa kweli kujiandaa , unachotakiwa ni kuwa imara kiakili.”
Orlando Pirates na Kaizer Chiefs watapambana Jumamosi uwanja wa FNB Jumamosi mchana.
 
Gary Neville amtolea uvivu Asern Wenger kuhusu Ozil
Gary Neville amemtolea uvivu meneja wa Arsenal Arsene Wenger kwa kushindwa kumpa muda wa kupumzika nyota wake Mesut Ozil katika kipindi cha mwisho wa mwaka yaa kipindi cha sikukuu za krismass na mwaka mpya ambapo alitolea mfano Cristiano Ronaldo mara kadhaa alikuwa akipewa mapumziko ya kipindi cha mapumziko nyakati kama hizo wakati huo akiwa na Sir Alex Ferguson enzi zake ndani ya United.
Ozil sasa anatarajia kuanza mapimziko ya wiki chache baada ya baada ya kukumbwa na matatizo ya msuli hapo jana katika mchezo wa ligi ya ambingwa Ulaya dhidi ya ambapo walitolewa rasmi mashindano usiku wa jana.
Kiungo huyo mjerumani alikuwa akionekana kufanya vema katika mchezo muhimu wa robo fainali ya FA ambapo Arsenal walishinda bao 4-1 dhidi ya Everton Jumamosi lakini amekuwa akilalamikiwa kwa kutojituma katika michezo mikubwa tangu kuanza kwa mwaka.
Neville ametumia mtandao wake wa kijamii wa Twitter kuweka wazi mawazo yake juu ya maamuzi ya Wenger kuendelea kumtumia Ozil katika kipindi chote cha krismass.
Ujumbe wake wa mtandaoni umesomeka
'Mwili wake unaonyesha wazi kuwa amekuwa akipambana ilhali akili ikiwa imechoka, hata hivyo ni jambo zuri kwani atakapo rejea atakuwa na nguvu mpya!
 
FA ya Sierra Leone kuchunguza ugomvi Rais wa soka nchini humo Johansen na nahodha wa zamani Kallon
 Chama cha soka nchini Sierra Leone (SLFA) linajipanga kufanya uchunguzi juu ya sakata la baina ya Rais wa chama hicho Isha Johansen na nahodha wa zamani wa nchi hiyo Mohamed Kallon.
Maamuzi hayo yanakuja siku moja baada ya Kallon mwenye umri wa miaka 34,kushikiliwa na polisi  kwa takribani masaa saba kwa mahojiano kabla ya kuachiwa baada ya kutoa dhamani ya dolari za kimarekani $11,000.
Tukio hilo lilitokea machi 6 baada ya mechi ya mchezo wa FA iliyohusisha timu ya Kallon, FC Kallon Junior, mjini Freetown.
Nyota huyo wa zamani wa Inter Milan na Monaco, Kallon alilalamikia kuchapwa kibao kwa nyuma ya shingo na Johansen baada ya mchezo.
Johansen baadaye akalalamika kuwa alikuwa akijitetea kuwa alikuwa katika hali ya kujitetea baada ya kusukumwa na Kallon ambaye pia alimtukana.
Kallon alipeleka lalamiko polisi lakini Jumatatu alishikiliwa kwa mahojiano chini ya inspekta msaidizi wa pilisi Al Sheikh Kamara ambaye alisema kuwa mchezaji huyo wa zamani alikuwa na tuhuma za kujibu juu ya hilo.
On Wednesday, the SLFA released a statement saying the matter had been referred to its disciplinary board. BBC Sport understands that the SLFA executive committee has also recommended for the matter to be dropped by police and dealt with by the governing body.
Baada ya Kallon kuhijiwa na polisi, wakili wake Emmanuel Saffa Abdulai alikaririwa akisema
"nimeshangazwa na kushitushwa na maamuzi ya polisi kumshikiliwa Kaloon, hili ni jambo la kushangaza kwakuwa mteja wangu ndiye aliyepaswa kuwa mlalamikaji sio mlalamikiwa katika tukio hili kwasababu yeye ndiye aliyepigwa kofi na ndiye alikuwa wa kwanza kushitaki polisi juu ya jambo hili.
"Mteja wangu amefanyiwa visivyo, mfumo huu wa sheria wa Sierra Leone unawapendelea wenye pesa."
Johansen amekataa kutoa maoni yake kwakuwa sahauri hilo liko kwenye uchunguzi wa polisi.
Kumekuwepo na mahusino mabovu baina ya Kallon na Johansen tangu uchaguzi wa SLFA uliofanyika mwaka 2013. Wawili hao waliteuliwa kwa ajili ya kinyang’anyiro cha uchaguzi wa Urais kabla ya Kallon na mgombea mwingine Rodney Michael kuenguliwa kwa kile kilechoitwa kuwa ni kukosa sifa kwa mujibu wa kamati maalum fifa ambapo baadaye Johansen alichaguliwa bila kupingwa.
 
Balotteli kikaaangoni Milan kiwango champonza
 Mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli ameingia katika lawama nzito kutoka kila upande wa vyombo vya habari vya Italia kufuatia kiwango chake kibovu katika michezo yote miwili ya klabu bingwa ulaya dhidi ya Atletico Madrid .
Bingwa mara saba wa vilabu binngwa Ulaya walitolewa katika michuano ya hiyo baada ya kufurushwa kwa kichapo cha mabao ya jumla 5-1 na Atletico Madrid, ambao waliwachapa Milan bao 4-1 hapo jana usiku.
The Gazzetta dello Sport lilimkosoa Balotelli baada ya kushindwa kuonyesha ubora wake katika michezo yote miwili likiwa na kichwa cha habari "Balotelli remains switched off,'' .
The Corriere dello Sport likiandika
"Terrible performance by the Rossoneri. Kaka goal, Balotelli disaster.''
Clarence Seedorf, ambaye alichukua kazi ya kuinoa Milan mwezi January baada ya kufukuzwa mtangulizi wake Massimiliano Allegri, pia ameingia katika ulingo mbaya wa ‘under fire’.
Safu ya tahariri ya Gazzetta dello sports imekuwa akilalamikia juu ya mbinu za ufundishaji za Seedorf na tabia ya Balotelli kimchezo likisema "Balotelli and Seedorf are also under scrutiny yaani wako chini ya uangalizi.''

No comments:

Post a Comment