KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, March 3, 2014

Real Madrid walipambana na vurugu za Atletico,tulikuwa tunataka sare tu. Anasema Carlo Ancelotti

Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti kumbe aliwataka wachezaji wake kukabiliana na watukutu wa Atletico jana katika hali yoyote ili angalau kupata alama muhimu ambayo itaendelea kuwaweka katika usukanani wa ligi kuu ya Hispania La Liga. 

Bao la dakika za mwisho lililofungwa na Cristiano Ronaldo liliwaokoa Real Madrid angalau kupata sare ya mabao 2-2 katika mchezo mgumu maarufu kama 'Madrid derby' katika dimba la Vicente Calderon hapo jana Jumapili. 

Matokeo hayo yana maanisha kuwa Real wako mbele kwa alama moja dhidi ya wapinzani wao wakubwa Barcelona. 

"Wao [Atletico] walikuwa wanajaribu kucheza mchezo wa vurugu. Tulijaribu kucheza na hatimaye tukafanikiwa kupata sare" Amesema Ancelotti.
"Tuemepata sare katika mchezo ambao pengine tungepoteza.
Atletico Madrid assistant coach German Burgos
Kocha msaidizi wa Atletico Madrid German Burgos akipozwa na kurejeshwa kutoka kwa mwamuzi ambapo alikuwa akimlalamikia mwamuzi wakati wa mchezo dhidi ya Real jana.
"Uwajibikaji ulikuwa mzuri na mwisho wa yote tunaweza kuridhika kwasababu Atletico ni wazuri hususani wanapokuwa katika uwanja wa nyumbani

No comments:

Post a Comment