Kocha Mkuu mpya wa Yanga Marcio Maximo (kushoto)akiwa na Afisa Habari Baraka Kizuguto, Katibu Mkuu Beno Njovu na kocha msaidizi Leonadro Neiva mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa JK Nyerere |
Kocha Mbrazil Marcio Marcel Maximo tayari ameshawasili jijini Dar es
salaam kwa ajili ya kuanza kazi kukinoa kikosi cha timu ya Young
Africans kwa ajili ya msimu ujao kwenye mashindano ya Ligi Kuu ya
Vodacom pamoja na mashindano ya Kimataifa.
Kocha Maximo ambaye awali aliwahi kufanya kazi nchini akiwa kama
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) amewasili mchana wa
leo akiwa na msaidizi wake Leonadro Martins Neiva kwa shirika la Ndege
la Afrika Kusini na kulakiwa na umati mkubwa uliokuwa umejitokeza
kumlaki.
Mara baada ya kuwasili kocha Maximo pamoja na msaidizi
wake Neiva walipokelewa na Katibu Mkuu wa Yanga SC Bw. Beno Njovu ambapo
mara baada ya kukamilisha masuala yote ya uhamiaji walitoka nje na
kuwapungia mikono washabiki, wapenzi na wanachama waliokuwepo uwanjani
hapo
Kuhus ujio wake Tanzania kujiunga na klabu ya Yanga SC Maximo
alisema kesho ataongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu
mitaa ya Twiga/Jangwani majira ya saa 5 kamili asubuhi ambapo ndipo
atapata fursa ya kueleza kila kitu juu ya ujio wake.
Aidha kesho
majira ya saa 8 kamili mchana kiungo mshambuliaji Andrey Macrcel Ferreira
Coutinho anatarajiwa kuwasili kwa shirika la Ndege la Afrka Kusini
tayari kwa ajili ya kujiunga na kikosi cha Young Africans kwenye
maandalizi ya msimu mpya wa 2014/2015.
Wapenzi, wanachama, na
washabiki wa Young Africans mnaombwa kujitokeza kwa wingi Uwanja wa
Ndege wa JK Nyerer kumpokea kiungo huyo ambaye amesema anakuja kufanya
kazi nzuri nchini na kuisaidia Yanga kwenye michuano mbalimbali.
No comments:
Post a Comment