Mgombea nafasi ya uraisi wa klabu ya Simba Evance Elieza
Aveva hii leo ameziundua rasmi kampeni za kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa
klabu hiyo ambao umepangwa kufanyika mwishoni mwa juma hili jijini Dar es salaam.
Evance Aveva ambaye anawani nafasi ya uraisi sambmaba na
mpinzani wake Andrew Tupa amesema kukubwa ambacho atakipigania endapo atapata
ridhaa kutoka kwa wanachama ni kuhakikisha umoja unarejea ndani ya Simba na kasha
masuala mengine ya kimaendeleo yatafuata.
Amesema kwa sasa klabu bya Simba imekosa sifa ya kuwa na
umoja miongoni mwa wanachama hali ambayo imekua chanzo cha baadhi ya mambo
kuharibika kuanzia nje hadi ndani ya uwanja na kupelekea timu yao kufanya
vibaya kwa miaka mitatu mfululizo.
Hata hivyo Aveva akasisitiza kwa kuweka mkazo suala la klabu
ya simba kurejesha hadhi yake ya kucheza soka kama ilivyokua miaka ya nyuma na
kufikia hadhi ya kutamba katika michuano ya kimataifa.
Amesema siri ya kurejewa kwa mafanikio hayo ni kutengeneza
kikosi cha wachezaji kwa kuangilia mpango wa muda mrefu na mfupi.
Katika hatua nyingine aliyekuwa mwenyekiti wa simba kabla
ya uongozi unaomaliza muda wake kuingia madarakani mwaka 2010, Hassan Dalali
ambae yupo bega kwa bega na Evance Aveva amewataka wagombea nafasi mbali mbali
wa klabu hiyo kuacha kasumba ya kuchafuana katika kipindi hiki cha kampeni na
badala yake watumie nafasi ya kuomba kura kistaarabu.
Wakati huo huo Gefrey Nyange Kaburu anaewani nafasi ya
makamu wa raisi wa klabu ya Simba nae amezindua kameni zake rasmi hii leo
ambapoa ameahidi kuendeleza mazuri ndani ya klabu hiyo endapo atapata nafasi ya
kuchaguliwa na wanachama siku ya jumapili.
Nae swed Nkwabi ambae anawani nafasi ya makamu wa raisi wa
klabu ay Simba amezindua kampeni zake hii leo mitaa ya kariakoo jijini Dar es
salaam, ambapo kubwa aliloliahidi ni kurejesha umoja na mshikamano ndani ya
klabu ya Simba.
No comments:
Post a Comment