Mwenyekiti wa SPOTANZA Abeid Kasabalala |
Chama cha wachezaji wa mpira wa Miguu nchini SPUTANZA
kimeendelea kusisitiza suala la kuingilia kati mikataba ya wachezaji ambao ni
wanachama wa chama hicho na klabu watakazosajiliwa kwa lengo la kulinda maslahi
yao ya sasa pamoja baadae.
Katibu msaidizi wa SPUTANZA Abeid Kasabalala amesema
mwishoini mwa mwezi May walitoa tamko la kuwa makini katika mikataba ya
wachezaji hususan katika kipindi hikia mbacho wachezaji wengi wamekua wakifanya
makubaliano na klabu wanazokubali kuzitumikia kwa ajili ya msimu mpya wa ligi.
Mwenyekiti wa klabu ya Simba Ismail Aden Rage aking'aka juu ya usajili wa mlinzi Kelvin Yondan aliyetokea Simba na kujiunga na Yanga usajili uliokuwa na utata |
Amesema kwa kipindi kirefu wamekua kimya na wameshuhudia
namna wachezaji wanavyo dhulumiwa haki zao stahiki, hivyo wameamua kuingia
kikamilifu katika harakati za kuhakikisha kila mchezaji anajua haki zake
kimkataba.
Katika hatua nyingine Abeid Kasabalala akawataka viongozi
wa klabu za ligi kuu pamoja na ligi daraja la kwanza kuwa na utaratibu mzuri wa
kuendesha klabu zao, kwa lengo la kuwajengea mazingira mazuri wachezaji
wanaowaandaa kwa ajili ya msimu mpya wa ligi.
Kasabalala ametoa rai hiyo kwa viongozi wa klabu kupitia
klabu ya Simba ambayo kwa sasa ipo katika harakati za kufanya uchaguzi pamoja
na usajili wa wachezaji.
No comments:
Post a Comment