Mabingwa wa ligi ya FA nchini Uingereza Manchester
City wamemsajili mchezaji wa kiungo cha kati Fernando Franncisco Reges kutoka kilbu ya
Porto kutoka Ureno.
Klabu hiyo ya Porto ndio iliyotangaza
makubaliano hayo katika soko la hisa la Lisbon siku ya jumatano baada ya
kukubali kumuuza mchezaji huyo kwa takriban paundi millioni 12.
City imethibitisha mpango huo siku ya alhamisi ijapokuwa maelezo ya makubaliano hayo hayakuwekwa wazi.
''Nitacheza uwezo wangu kila ninapokuwa katika
uwanja na ninataraji kuichezea kilabu hiyo kwa miaka mingi
ijayo.',alisema Fernando.
''Ninafurahia kuwa katika kilabu hii na natamani kucheza katika ligi ya Uingereza''.
Kwa mara ya kwanza mchezaji huyo alihusishwa na
timu ya City mnamo mwezi January na ni mchezaji wa pili kusajiliwa na
kilabu hiyo baada ya kumsajili beki wa kulia wa Arsenal Bacary Sagna.
''Nina furahi kujiunga na Manchester
City'',aliongezea.Najua kulikuwa na mazungumzo ya mimi kusajiliwa na
City mnamo mwezi January ,kwa hivyo ninafurahi kwamba makubaliano hayo
sasa yameafikiwa na kwamba mimi ni mchezaji wa City.
No comments:
Post a Comment