Yametimia: Herrera akionyesha jezi ya United akiwa na Sir Bobby Charlton baada ya kukamisha uhamisho wenye thamani ya pauni milioni £29 |
Manchester United imekamilisha usajili wa Ander Herrera kwa pauni milioni £29 baada ya kukubali kuuvunja mkataba wake ndani ya Athletic Bilbao.
Bilbao inayoshiriki ligi kuu ya Hispania 'Liga club' hapo awali iligomea ombi la timu ya Louis van Gaal United, lakini baada ya kiungo huyo wa kati kufanikiwa katika vipimo ndani ya Carrington Jumatano, mpango hatimaye umekubalika rasmi.
Akiwa na umri wa miaka 24 Herera anathibishwa na United kuwa mchezaji wa kwanza kusajili na Van Gaal aliyechukua nafasi hiyo ya umeneja Old Trafford kutoka kwa David Moyes.
Nje ya viunga vya Carrington: Kiungo Herera anapeana mikoni na muasisi Sir Bobby Charlton
Herrera akipiga picha ya kumbukumbu katika nembo kubwa ya uwanja wa mazoezi wa United Carrington
Taarifa ya Bilbao mbali ya kutangaza rasmi juu ya maamuzi yake hayo ya kumuachia kiungo huyo pia imemshukuru kiwa utumishi wake wa miaka mitatu
No comments:
Post a Comment