KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, July 7, 2014

Kocha wa Algeria ajiuzulu na kukataa ombi la Rais Abdelaziz Bouteflika

Vahid Halilhodzic amejiuzulu licha ya ombi la Rais Bouteflika asijiuzulu
Kocha wa Algeria Vahid Halilhodzic amejiuzulu kazi hiyo licha ya ombi la kibinafsi kutoka kwa rais Abdelaziz Bouteflika akimsihi asijiuzulu.
Vahid ambaye amekuwa Kocha wa timu ya Algeria kwa takriban miaka mitatu na hapo awali meneja wa timu ya Ivory Coast, alikataa ombi hilo akidai kuwa kuna changamoto za kimichuano.
Vahid ambaye ni mzaliwa wa nchi ya Bosnia aliipeleka Algeria  mpaka kufikia hatua ya mtoano ya michuano ya kombe la dunia nchini Brazil kabla ya kutolewa kishujaa na Ujerumani.
 Timu yake ilikuwa imesalia kati ya timu zingine kumi na sita bora katika hatua hiyo ya kombe la dunia.
Timu ya Algeria baada ya kuilaza South Korea mabao manne kwa mawili, haikufanikiwa kupona katika hatua ya mtoano baada ya kulazwa mabao mawili kwa moja dhidi ya timu ya Ujerumani.
Hapo awali, katika michezo ya ufunguzi, Algeria ililazwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Belgium, na kutoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Urusi na kufuzu kwenda raundi ya pili.

No comments:

Post a Comment