KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, September 8, 2014

Serena ashinda taji la 18 la Grand Slam


Williams akilala chini kwa furaha uwanja wa Arthur Ashe Arena baada ya kumshinda Caroline Wozniacki
Mcheza tennis Serena Williams wa Marekani ametwaa ubingwa wa US Open.
Williams ameshinda katika mchezo uliofanyika usiku wa kuamkia leo baada ya kumtwanga Caroline Wozniacki wa Denmark kwa ushindi wa moja kwa moja.

Mpambano huo wa fainali ulipigwa mjini New York ambapo Serena ameshinda kwa seti 6-3, 6-3 na kujinyakulia ubingwa huo kwa mara ya 6.

Kwa sasa Serena ndiye mchezaji nambari 1 duniani kwa mchezo huo na pia bingwa mara 18 wa Grand Slam, amekuwa bingwa wa kombe hilo mara tatu mfululizo tangu mwaka 2012.

Wozniacki ambaye ni rafiki wa karibu wa Serena alimpongeza rafiki yake huyo baada ya mchezo na kusema alistahili ushindi huo kutokana na jinsi alivyocheza.
Over the moon: Serena Williams celebrates her US Open victory with a jump for joy with the trophy
Serena Williams akishangilia ushindi wa US Open dhidi ya Caroline.
Overwhelmed: Serena Williams drops to the court after beating Caroline Wozniacki for the US Open title
Serena Williams akianguka kwa furaha baada ya kumchapa Caroline Wozniacki katika US Open
Formidable: Williams dominated as she claimed an 18th career Grand Slam title
Passion: Williams screams in anguish despite being well in control of the match from the outset 
Out of reach: Wozniacki stretches for a forehand as she falls to Williams in 75 minutes
Kashindwa kufikia malengo: Wozniacki akijinyoosha msuli dhidi ya Williams dakika ya 75
Good spirits: Wozniacki and Williams share a laugh after the presentation in New York
Wozniacki na Williams wakionyesha tabasamu jijini New York

No comments:

Post a Comment