KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, February 19, 2014

Pep Guardiola: NI VIGUMU KUDHIBITI DAKIKA 90 DHIDI YA ARSENAL

Kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola amekiri ni vigumu sana kudhibiti dakika tisini za mechi ya aina yeyote dhidi ya Arsenal ya Uingereza .

Guardiola

"Uunaweza cheza vizuri na utawale nyanja zote kwa dakika 30 ama 75 hivi lakini zile zitakazosalia utakabiliwa na upinzani mkali "
Guardiola ambaye hajashinda katika mechi zake mbili uwanjani Emirates ,anatarijia ushindani mkali .
Licha ya hayo , Bayern Munich imeshindwa katika mechi mbili pekee msimu huu.
Bayern ilishindwa na Borussia Dortmund na Manchester City mapema katika mkondo wa kwanza wa ligi ya msimu huu.
Mwaka uliopita Bayern,iliilaza The Gunners 3-1 katika hatua hii ya Robo fainali.
Hata hivyo vijana wa Pep walifuzu kutokana na sheria ya bao la ugenini licha ya kushindwa 2-0 katika mkondo wa marudiano huko Ujerumani.

Vijana wa Arsene Wenger hawajahi kushinda taji lolote tangu mwaka wa 2005 lakini Guardiola anasisitiza kuwa sio timu hafifu kamwe.

No comments:

Post a Comment