KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, October 10, 2014

Ukurasa mkubwa wa kimataifa: Roy Kean kumbwatukia Ferguson uso kwa uso kisa nini? Laurent Koscielny naye apata majeraha na kuongeza maumivu kwa Arsene Wenger, Robert Pires amshauri Wenger kumununua Sami Khedira mwenzi Januari kwa kuwa ana vitu kama Patrick Viera, Luis Saurez atakuwa nyota kuliko Messi na Neymar na nyingine kibao................................



Mchezaji wa zamani wa timu ya Manchester United Roy Keane amesema kuwa aliyekuwa kocha wa kilabu hiyo alikosea kuwashtumu wachezaji wake wa zamani katika wasifu wake na kwamba haogopi kumkaripia iwapo wawili hao watakutana.

Ferguson alizungumzia kuhusu wachezaji wa zamani wa kilabu hiyo Roy Kea na david Beckam katika kitabu hicho kilichochapishwa mwaka uliopita.Keane aliondoka Old trafford mwaka 2005 baada ya kukosana na Fergurson.

''Nahisi ni makosa makubwa kunishtumu mimi na wachezaji wengine'' Keane mwenye umri wa miaka 43 aliambia Footbal Focus.''tulifanya vyema katika kilabu hiyo ,tuliweza kupata mafanikio ,tulishinda mataji na sasa kocha anatushtumu.

''Meneja ambaye amejipatia mamilioni ya pauni kutokana na jasho letu,alikabidhiwa sanamu na maeneo yaliotajwa baada ya jina lake, na anafikiri anaweza kutushtumu bila mmoja wetu kusema lolote kwa kuwa anadhani ana mamlaka yote.

Nilisema haiwezekani,kwa nini tukubali kusikiza upuzi kama huu.katika kitabu chake Fergurson amedai kwamba Roy Keane ambaye alikuwa kiungo muhimu wa mafanikio ya timu katika miaka 12 aliyoichezea aliendelea kuwa na ushawishi mbaya.

Keane amesema kuwa hadhani kuwa anaweza kumsamehe Fergurson kwa matamshi yake na kuongezea kwamba hajali kusema lolote lililo moyoni mwake kwa meneja huyo wa zamani iwapo watakutana tena.



Laurent Koscielny naye apata majeraha na kuongeza maumivu kwa Arsene Wenger
Bundi wa majeraha ameendelea kudumu katika klabu ya Arsenal kufuatia beki Laurent Koscielny kulazimika kujiondoa kwenye mazoezi ya timu yake ya kitaifa ya Ufaransa kutokana na maumivu ya ukano wa kisigino.

Meneja Arsene Wenger amepigwa na pigo moja baada ya lingine ikiwa ni mechi saba tu ndani ya msimu mpya huku ambapo sasa Koscielny anajiunga na nyota wenzake Mathieu Debuchy, Mikel Arteta, Olivier Giroud, David Ospina, Aaron Ramsey na Yaya Sanogo kwenye zahanati.

Siku mbili baada ya Ujerumani kutangaza kiungo nyota Mesut Ozil atalazimika kutocheza kati ya wiki 10 na 12, Wenger ameongezewa tumbo joto na habari kuwa beki Koscielny amejiondoa kutoka mechi za Ufaransa dhidi ya Ureno na Armenia kwenye msururu wa kufuzu Kombe la Euro la 2016.

Shirikisho la Ufaransa limeandika kwenye anwani yao ya mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Koscielny anauguza uvimbe wa ukano wake wa kisigino.

 Frank Ribery kurejea uwanjani hivi karibuni
Mshambuliaji Franck Ribery anakaribia kurejea katika klabu yake ya Bayern Munch kufuatia kukosekana kwa kipindi kirefu.

Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa ameichezea klabu yake mchezo mmoja tuu msimu huu kufuatia kupata maumivu ya mguu.

Lakini hata hivyo mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 ambaye alilazimika kuikosa michezo ya kombe la dunia wakati wa kiangazi nchini Brazil kutokana na maumivu ya mgongo lakini sasa amerejea katika mazoezi baada ya kuponya matatizo ya msuli yaliyokuwa yakimsumbua.

Taarifa kupitia mtandao wa klabu yake imesema

"Franck Ribery anaendelea vizuri kuelekea kurejea kikosini.

Bayern bado wanaendelea kuikosa huduma ya Bastian Schweinsteiger, Thiago, Javi Martinez na Holger Badstuber kutokana na kukumbwa na majeraha na hivyo kukipa kikosi cha kocha Pep Guardiola wakati mgumu.

Kwasasa Bayern inaongoza ligi kuu ya Ujerumani Bunderliga wakiwa mbele kwa zaidi ya alama nne wakiwa na alama 17 baada ya michezo saba.

 Arsene Wenger kupanga ratiba ya matibabu ya Ozil baada ya mchezo wa kimataifa wa Ujerumani
MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema watapanga ratiba ya matibabu ya Mesut Ozil baada ya kiungo huyo kurejea kutoka katika majukumu ya kimataifa akiwa majeruhi.

Ozil anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi mitatu kutokana na majeruhi ya goti baada ya kufanyiwa vipimo akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani.

Lakini Wenger amesema mtaalamu wa klabu hiyo ndio atakaetoa ushauri wa jinsi gani ya kukabiliana na tatizo hilo wakati watakapotafuta utaratibu wa kumtibu haraka iwezekanavyo.

Wenger aliendelea kudai kuwa madaktari wa Arsenal nao wataangalia vipimo alivyofanyiwa na kutoa ushauri wao.

 Arsenal imeandamwa na majeruhi kadhaa msimu huu lakini Wenger amabinisha kuwa Theo Walcott na Serge Gnabry wote wanakaribia kurejea katika kikosi cha kwanza wakati Aaron Ramsey naye amebakisha siku nane kabla ya kuanza mazoezi.

 Robert Pires amshauri Wenger kumununua Sami Khedira mwenzi Januari kwa kuwa ana vitu kama Patrick Viera 
Robert Pires amemtaka Arsene Wenger kuwasha tena moto wa mataji  kwa Arsenal katika ligi kuu ya England ( Premier League) kwa kumsajili Sami Khedira kutoka katika klabu ya Real Madrid mwezi Januari.

Nyota huyo wa zamani wa washika mitutu wa anaamini kuwa klabu yake hiyo ya zamani inakosa kiungo bora mwenye sifa za aliyekuwa kiungo wakati wake Patrick Vieira.

Pires anaona sifa zilezile za ufiti na kujituma ndani ya Khedira, ambaye alikuwa akihusishwa kuelekea Arsenal wakati wa kiangazi ambaye sasa ameingia katika mwaka wake wa mwisho wa mkataba na Madrid.

Amekaririwa Pires akisema

“Wenger anahitaji mchezaji wa kiungo mwenye mwili mkubwa kama Vieira, mwenye nguvu, mrefu, kwasbaba nafasi hii ni muhimu kuunganisha ushambuliaji na ulinzi wa timu” Mfaransa huyo alikuwa akionge na gazeti la Daily Telegraph.

 “ubora upo, pengine mtu kama Yaya Toure katika kiungo. Ananikumbusha Patrick Vieira, lakini pengine wanayo fursa hiyo hiyo kwa Khedira.

Pires anaamini timu ya Wenger bado wananafasi ya kuwania taji ingawa Chelsea ndio walioanza vizuri msimu huku ikipata ushindi baina yao huko  Stamford Bridge.

“wanazidiwa na Chelsea kwa alama tisa lakini bado tunaweza kutwaa taji” Amesisitiza Pires.


 Luis Saurez atakuwa nyota kuliko Messi na Neymar
Mshambuliji Luis Suarez ni mchezaji ambaye atakuwa bora kuwazidi nyota wengine kama Lionel Messi na Neymar, hii ni kauli ya mkongwe wa Uholanzi Johan Cruyff.


Suarez aliyesajili wa kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £70 kiangazi kuelekea Barcelona akitokea Liverpool bado hajaanza kutoa huduma katika klabu yake hiyo mpya akiendelea na adhabu ya kusimama kwa miezi minne kufuatia kumtafuna Giorgio Chiellini wa Italia wakati wa kombe la dunia.

Hata hivyo Cruyff anasema  Suarez ni habari nyingine na tangu kutambulishwa Barcelona anamuona kama ni mtu ambaye ataamsha makali ya safu ya ushambuliaji ya Barca.

Anasema wakati wa kombe la dunia ni washambuliaji watatu ndio waliokuwa gumzo nchini Brazil akiwemo yeye Suarez.

Amekaririwa akisema

“Pengine uwepo wa Suarez utaimarisha muunganiko mzuri kati ya Messi na Neymar,”.

“Pamoja na Messi, wakati mwingine ni vigumu kufunga unahitaji usaidizi wa kufunga na Suarez ana ubora huo, msimu uliopita hatukuona muunganiko hivyo tutaona nini kitatokea  baadaye.

 Mchezaji wa kutumainiwa wa Guinea akimbia timu taifa kisa Ebola
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Guinea Alhassane Bangoura amefichua kwamba alijiondoa katika kikosi kitakachokabiliana na timu ya taifa ya Ghana kwa sababu mchezaji mwenzake wa timu ya Rayo Vallecano alihofia kwamba huenda akaambukizwa ugonjwa wa Ebola.


Mamia ya watu tayari wamepoteza maisha yao kutokana na virusi vya ugonjwa wa Ebola nchini Guinea hivyo basi taifa hilo limechukua hatua ya kuihamisha mechi yao ya kufuzu kwa kombe la taifa bingwa barani Afrika nchini Morocco hapo jumamosi.

"Nilimuomba mkufunzi wa timu ya taifa ya Guinea Michel Dussuyer kuniruhusu nijiondoe kwa sababu wenzangu waliogopa kwenda,'' Bangoura aliiuambia mtandao wa Rayo.

''Rayo haikuniambia chochote, maamuzi haya ni yangu binafsi''.

Mkurupuko wa Ebola unaoshuhudiwa kwa sasa ktika eneo la Afrika Magharibi umewaua watu wengi zaidi kuliko magonjwa mengine yote kwa pamoja, huku mataifa ya Guinea, Sierra Leone na Liberia yakiathirika zaidi.

Kama njia moja ya kuzuia kuenea kwa virusi vya Ebola, shirikisho la kadanda nchini Sierra Leone lilisitisha mechi zote za kadanda kufanyika.

Pia shirikisho la kadanda la bara Afrika (CAF) liliamuru mechi zote zinazohusisha timu za Sierra Leone, Guinea na Liberia zilizoratibiwa kuchezewa katika nchi hizo kuhamishwa katika nchi nyingine tofauti

Sierra Leone tayari imepata mataifa yatakayowaruhusu kuandaa mechi zake na wamewahakikishia kwamba wameweka mikakati kabambe ya kuhakikisha ugonjwa huo hauambukizwi wachezaji na wakufunzi.


Mataifa ya Afrika: Papiss Cisse kukiongoza kikosi cha Senegal dhidi ya Tunisia
Senegal inamatumaini mshambuliaji wake anayechezea katika klabu ya Newcastle United Papiss Cisse atacheza kwa kiwango cha juu kama anavyofanya katika ‘English Premier League’ watakapo ni wenyeji wa Tunisia mjini Dakari.


Cisse alikuwa bora katika mchezo uliomalizika kwa sare dhidi ya Swansea City wiki iliyopita na kurejea kwake kutoka katika maumivu ya mguu itasaidia kujazia pengo loa kukosekana kwa mshambuliaji mwingine wa Stoke City Mame Diouf, ambaye anasumbuliwa na msuli wa paja.

Senegal kwasasa ni moja kati ya timu za taifa ambazo zinamchezo mzuri barani Afrika ikiwa na alama sita walizovuna katika michezo miwili dhidi ya Misri huku ambapo nyota wa Lokomotiv Moscow Dame Ndoye akitoa mchango mkubwa katika kuzalishwa kwa mabao.

Mabingwa watetezi Nigeria watakuwa ugenini dhidi ya Sudan hapo kesho katika mchezo wa kundi A wakisaka ushindi wa kwanza katika kundi baada ya kufungwa kwa mshituko na Congo huku pia wakiwa na kumbukumbu ya sare dhidi ya Afrika kusini.


No comments:

Post a Comment