KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, October 9, 2014

Ukurasa wa kimataifa: Wayne Rooney ajitathimini upya na hasira zake, Diego Costa anasema yuko fiti


Wakala wa mchezaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo Jorge Mendes amesema kuwa mchezaji huyo hana nia yoyote ya kurudi Manchester United.
Ronaldo, 29, alikaa kwa miaka sita Old Trafford katika uchezaji wake wa soka, lakini hivi karibuni amekuwa akihusishwa na taarifa za kutaka kurejea kwenye klabu hiyo.
Ripoti katika vyombo kadhaa vya habari nchini uingereza vilisema kuwa dili hilo lililkuwa limepngwa kukamilika katika usajili wa mwaka 2015, kiasi cha kufikia mashabaiki wa united kutuma vipeperushi vya kuashiria kuridhia mchezaji huyo ambaye ni kipenzi chao kurejea klabuni hapo, na hivi karibuni mashabiki wa united walionekeana kwenye uwanja wa El Madriga ambapo Real walishinda bao 2-0 mwezi uliopita.
Ronaldo ambaye anashikilia tuzo ya Ballo , amefunga magoli 13 katika michezo sita ya La la liga msimu na kumuongezea kujenga uwezo zaidi.
Mendes amesema kuwa mteja wake hana dalili za kuondoka kwenye klabu hiyo yenye maskani yake Estadio Santiago Bernabeu, na wala hakuna klabu yoyote ambayo imekwishapiga simu ikihitaji huduma ya mchezaji huyo.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

 Wayne Rooney ajitathimini upya na hasira zake
Nahodha wa Manchester United na England Wayne Rooney amesema kwa sasa ni mtu mzima, lakini amekuwa akitafakari ni namna gani ataweza kuzuia hasira zake mchezoni.
Rooney, mwenye umri 28, amekosolewa vikali baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo wa ligi kuu soka England ambapo United iliibuka na ushindi wa bao 2-1 dhid ya West Ham uwanjani Old Trafford mwezi uliopita.
Rooney amesisitiza kuwa hivi sasa amebadilika tofauti na Yule wa zamani ambaye alikuwa na tabia ya kukasirika kila mara, hivyo amewataka radhi mashabiki wa united na kuongeza kuwa rafu aliyomchezea Stewart Downing haikuwa ya kiungwana.
 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
Mchezo wa AFCON wa Ghana dhidi ya Guinea kuchezwa Tamale
Chama cha soka cha nchini Ghana GFA, kimeamua mchezo wake wa AFCON 2015 kati ya Ghana na Guinea kuchezwa Tamale na si mjini Kumasi.
Rais FA nchini Ghana Kwesi Nyantakyi amekanusha tetesi zilizodai kuwa mchezo huo umehamishwa kutokana mapokezi hafifu ya mashabiki mjini Kumasi katika mchezo wa Ghana na Uganda uliofanyika katika mji huo, lakini ni utaratibu ambao wamejiwekea kwa ajili ya kuhakikisha miji yote inashuhudia mechi za kimataifa.
Katika upande mwingine Kwesi amesema kuwa nyumbani ni nyumbani, na uwanja wa Kumasi haujatelekezwa moja kwa moja kwani wengine walishauri michezo mingine ya Ghana kuchezwa Togo lakini Nyumbani ni Nyumbani.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
Denis Oliechi kuungana na Harambee Stars

Mchezaji wa kimataifa wa Kenya anaecheza soka la kulipwa nchini Ufaransa Dennis Oliech hatoweza kujumika katika kikosi cha Harambee Stars kitakachosafiri kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya MOrroco utakaopigwa mjini Marrakech jumatatu ya October 13, 2014.

Kulingana na kocha wa timu hiyo Bobby Williamson, Oliech, ambaye alikuwa nchni Kenya kwa sababu binafsi yuko katika kambia kwa ajili ya kupasha mwili joto na wenzake kwa nia ya kujiweka fiti.

Kocha Bobby Williamson amekaririrwa akisema kuwa, Oliech yuko na wenzake katika kambi ya timu ya tiafa ya Kenya lakini si mmoja ya wale wataongozana na timu kuelekea nchini Morroco, lakini aliomba ruhusa ya kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiweka fiti kabla ya kurudi katika klabu yake hukio Ufaransa.
Oliech kwa sasa hayuko katika mipangio ya kocha Williamson katika kikosi cha sasa ila amempa nafasi ya kurudi kikosini katika majukumu mengione ya kimataifa hususani kwenye michuano minine ya kimataifa.
Williamson anataraji kukipunguza kikosi chake cha sasa kutoka wachezaji 26 mpaka 19 watakaondoka ijumaa, na watakaobaki watakuwa ni sehemu ya timu hiyo.
@@@@@@@@@@@@@@

Diego Costa anasema yuko fiti

Diego Costa ameonyesha kutosumbuliwa na tatizo lolote la maumivu ya misuli ya paja baada ya kuanza mazoezi na timu ya Hispania kwa mafanikio ya kujiandaa na michezo ya kufuzu kwa Euro 2016 dhidi ya Slovakia na Luxembourg.
Msambuliaji huyo wa Chelsea amejiunga na mchezaji mwenzake Cesi Fabregas wanaotoka klabu moja, pamoja na nyota wengine wanoacheza ligi soka England akiwemo David Silva na golikipa David de Gea wa Manchester.
Timu hiyo inayofundishwa na kocha mkongwe Vicente del Bosque, iliitandika Macedonia goli 5-1 katika mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo, na sasa ni zamu ya Slovakia pamoja na Luxembourg.
Costa, amefunga magoli tisa katika mechi saba za ligi kuu soka England, akichezea klabu yake ya Chelsea msimu huu, lakini amekuwa na wakati mgumu kupachika magoli akiwa na kikosi cha Hispania katika michezo ya kimataifa hivyo ni wakati mwingine wa mchezaji huyo kuonyesha makali yake katika michezo hiyo miwili ya juma hili.
Wakati huo huo Kocha Del Bosque, amesema kuwa hashangazwi na timu yake kushindwa kuonyesha kiwango cha hali ya juu katika michuano ya kombe la dunia huko Brazil, na kuongeza kuwa timu hiyo iko katika kipindi cha mpito licha ya kupoteza muelekeo katika michuano hiyo mikubwa.
Hata hivyo amewataka wachezaji wake kusahau yaliyopita huko Brazil, kwani hivi sasa ana damu mpya ambazo zina ari ya kutaka kufanya makubwa, ni bora wakawaza mwanzo mpya.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

No comments:

Post a Comment