KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, August 5, 2010

Taarifa hii ni kwa hisani ya blog ya full shangwe
usiku wa jana kuamkia leo timu ya taifa wanawake ya tanzania ilikuwa dimbani ikicheza dhidi ya timu ya akina dada wenzao wa marekani ya Northwest National Reds ambayo ina wachezaji wenye umri wenye umri chini ya miaka 18 ukiwa ni mchezo wa kirafiki mchezo ukipigwa katika dimba la Starfire Sports Complex south of Seattle, Washington, USA.
katikamchezo Twiga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 licha ya kusafiri kwa muda mrefu huku mabao ya Twiga yakifungwa na Eto Mlenzi na Esther "Lunyamila" Chabruma.
timu hiyo ni moja kati ya timu za vijana za akina dada wa Marekani na wachezaji wake wengi wakitokea katika vyuo vya elimu ya juu. timu hiyo inadhaminiwa na Ms. Rahma Al-Kharoosi, kupitia kampuni yake ya RBP Oil & Industrial Technology Ltd.
wanataraji kushuka tena dimbani August 7 kucheza dhidi ya akina dada wengine wa Seattle Sounders Women's Team, ambao timu yao inashiriki ligi ya Marekani maarufu kama USL W-League, ukiwa ni mchezo wao wa pili. lengo la ziara hiyo ni kujiweka fiti kabla ya maandalizi yao ya African Women's Championship ambayo inatarajiwa kufanyika nchini Afrika kusini mwezi October.
Twiga Stars imefuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika baada ya kuichapa Ethiopia 4-2 on ukiwa ni ushindi wa jumla na baadaye kuichapa 11-3 ushindi wa jumla . http://www.twigastars.com/


mchezi

No comments:

Post a Comment