KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, June 29, 2012

Balotelli: Mabao yote ni kwa ajili ya mama yangu. Ulikuwa usiku bora katika maisha yangu

Super Mario Balotelli akipongezwa baada ya kufunga bao la pili la Italia

Mario Balotelli ameutaja usiku wa jana kuwa ulikuwa ni wa kipekee katika maisha yake baada ya kuisaidia timu ya taifa lake la Italia kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ujerumani ushindi ambao umekivusha kikosi cha kocha  Cesare Prandelli kutinga fainali ya Euro 2012.
Balotelli alikuwa katika usiku wa kipekee uliokuwa bora kimchezo katika maisha yake ya soka akiwa amevalia jezi ya rangi ya blue akifunga mabao mawili la kwanza la kichwa kufuatia kross ya Antonio Cassano na bao la pili baada ya kupokea pasi ya kutanguliziwa na Riccardo Montolivo.
Mshambuliaji huyo wa Manchester City amekuwa akiandamwa na vyombo vya habari katika fainali hizi hususani baada ya kupigiwa kelele na meneja wake kuwa kiwango chake kilishuka hususani katika mchezo mwisho wa hatua ya makundi dhidi ya Ireland.
Lakini baada ya yote hayo jana alionekana akiwa na tabasamu ambalo huwa ni nadra kuonekana hivyo baada ya mabao yake mawili kutosha kubariki safari ya Italia kucheza fainali ya Euro 2012 baada ya kuikosa kwa miaka 12.
Amenukuliwa akisema
“huu ulikuwa ni usiku wa furaha na aina yake katika maisha yangu lakini nadhani jumapili itakuwa zaidi,”.
“natumaini kushinda , sijali kama nilicheza vibaya kwa kuwa tulijituma . sasa tunapumzika , hatupaswi kujichanganya kuhusiana na mchezo wa Hispania wa kutawala mchezo sisi tunacheza mpira wetu.
Balotelli amesema magoli aliyofunga yalikuwa ni maalum kwa mama yake ambaye alisafiri kutoka Italia kwenda kuona mchezo huo.
“Baada ya mchezo nilikwenda kwa mama ilikuwa rah asana nilimwambia mama haya ni kwa ajili yake,” .
“nilikuwa nasubiri kipindi kama hiki kwa muda mrefu ukizingatia mama yangu si kijana tena hawezi tena kusafiri mbali kwa hiyo ilikuwa ni kumfanya mwenye furaha kusafiri mpaka hapa. Baba yangu atakuwepo katika mji wa Kiev katika mchezo wa fainali.

“kabla ya mchezo kulikuwepo mama yangu, kaka zangu,shemeji yangu na rafiki yangu kipenzi. Ukaribu wao na mapenzi yao ni wazi viliniripua . Unajua nilikuwa nasikiliza wimbo gani kabla ya mchezo? Drake. He’s a friend of mine."
    “Mwisho wa mchezo nilikwenda kwa mama aaaaaaaaaah ilikuwa  that was the best moment. Nilimwambia magoli haya ni kwa ajili yake” hiyo ni kauli ya Mario Balotelli

Mabao ya Balotelli ya jana yana muunganisha na wafungaji wengine wenye magoli mengi katika fainali hizi  Cristiano Rolando, Mario Mandzukic na Mario Gomez lakini katika wote hao ni yeye aliyesalia katika mashindano.
Anaendelea kunukuliwa akisema
“nitajaribu kushinda tuzo ya mfungaji bora . katika soka mara nyingine unaweza kujaribu mara nyingi na mambo yasiende kama unavyo tarajia na ukajaribu mara chache na ukafanikiwa " .

No comments:

Post a Comment